Sunday 31 May 2009

MMILIKI NEWCASTLE ATAKA KUTIMKA!!

Mike Ashley anaemiliki Klabu ya Newcastle amesema anatafuta mnunuzi wa Klabu hiyo mapema iwezekanavywo. Ashley hivi juzi aliwaomba radhi Mashabiki kwa makosa yaliyofanyika Misimu miwili iliyopita mpaka yakasababisha timu kuporomoka Daraja. Ashley amekiri: 'Ni balaa kubwa kwa kila mtu! Nimepoteza pesa zangu na nilifanya maamuzi mabovu! Sasa nataka kuiuza Klabu na Washauri watateuliwa hivi karibuni!'
Mike Ashley amekiri ilikuwa ni kosa kubwa kwake aliponunua asilimia mia ya hisa za Klabu hiyo. Ashley anasema: 'Hilo ni kosa! Najuta kwa sababu mie sie mtaalam wa soka! Mie ni Shabiki tajiri tu!'

No comments:

Powered By Blogger