Friday 5 June 2009

Gattuso ndani ya Italia Bondeni!!
Kiungo wa AC Milan Gennaro Gattuso ametajwa na Meneja wa Italia Marcello Lippi kuwa ni mmoja wa Wachezaji 23 wa Italia watakaoshuka Bondeni, huko Afrika Kusini, kushindania Kombe la Mabara la FIFA wiki ijayo wakiwa Kundi moja pamoja na Watetezi wa Kombe hilo Brazil, USA na Mabingwa wa Afrika Egypt.
Gattuso hajacheza karibu msimu mzima baada ya kuumia goti lakini kwa mshangao wa wengi yupo Kikosini pamoja na Fulbeki chipukizi Davide Santon [18] wa Inter Milan na Mshambuliaji aliekulia Manchester United Giuseppe Rossi anaechezea Villarreal.
Mwingine ambae uteuzi wake ni wa kushangaza ni Andrea Dossena wa Liverpool.
KIKOSI KAMILI:
Gianluigi Buffon (Juventus), Marco Amelia (Palermo), Morgan De Sanctis (Galatasaray); Fabio Cannavaro (Juventus), Giorgio Chiellini (Juventus), Gianluca Zambrotta (Milan) Fabio Grosso (Lyon), Davide Santon (Inter), Alessandro Gamberini (Fiorentina), Nicola Legrottaglie (Juventus), Andrea Dossena (Liverpool); Mauro Camoranesi (Juventus), Gennaro Gattuso (Milan), Angelo Palombo (Sampdoria), Riccardo Montolivo (Fiorentina), Daniele De Rossi (Roma), Andrea Pirlo (Milan); Alberto Gilardino (Fiorentina), Vincenzo Iaquinta (Juventus), Fabio Quagliarella (Napoli), Luca Toni (Bayern Munich), Giuseppe Rossi (Villarreal), Pepe (Udinese)

No comments:

Powered By Blogger