Sunday 31 May 2009

HIDDINK ABEBA FA CUP NA KUIAGA CHELSEA!!
Guus Hiddink, Mdachi aliyeletwa na Roman Abramovich ili kuiokoa Chelsea Februari mwaka huu baada ya kufukuzwa Kocha wa Dunia, Mbrazil, Luis Felipe Scolari, ametimiza ahadi yake na kuibebesha Chelsea Kombe la FA.
Hiddink amekubali: 'Hili ni Kombe muhimu na ni historia kuchukua! Nimefanya kazi na watu wema! Wachezaji wazuri kabisa!'
Nahodha wa Chelsea, John Terry, akaungama: 'Ni miaka miwili hatuna Kombe! Timu nzima tumempa zawadi! Tumewaona Man U wanachukua Vikombe kaja yeye tumepata!'
Frank Lampard akamalizia kwa kutoa kauli ya wenzake kwamba: GUS HIDDINK ni MTU MKUBWA, MTUKUFU NA KOMBE HILI ANASTAHILI YEYE!!

No comments:

Powered By Blogger