Saturday 6 June 2009

KAZAKHSTAN 0 ENGLAND 4
England ikicheza ugenini Uwanja wa Almaty Central huko Almaty, Kazakhstan wamewafunga wenyeji wao Kazakhstan mabao 4-0 kwenye mechi ya Kundi la 6 la Nchi za Ulaya kugombea nafasi za kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwaka ujao 2010.
Mabao ya England yalifungwa na Gareth Barry na Emile Heskey kwenye kipindi cha kwanza na kipindi cha pili Wayne Rooney akapachika la 3 kisha Frank Lampard akafunga bao la 4 kwa njia ya penalti baada ya Heskey kuchezewa faulo.
England Jumatano ijayo nyumbani kwao Wembley, London watacheza mechi nyingine ya Kundi lao na Andorra.

England ndie anaeongoza Kundi hilo kwa kuwa na pointi 18 akifuatiwa na Croatia, anaecheza baadae leo na Ukraine, akiwa na pointi 10.
KIKOSI CHA ENGLAND: Green, Johnson, Terry, Upson, A Cole, Walcott, Barry, Lampard, Gerrard, Rooney, Heskey.AKIBA: Robinson, Lescott, Bridge, Defoe, Wright-Phillips, Beckham, Crouch.
MATOKEO KOMBE LA DUNIA:
NCHI ZA ASIA:
NORTH KOREA 0 IRAN 0
UZBEKISTAN 0 JAPAN 1
NCHI ZA AFRIKA:
ZAMBIA 1 RWANDA 0
MALAWI 0 BURKINA FASO 1
GABON 3 TOGO 0

No comments:

Powered By Blogger