Sunday 7 June 2009

Uholanzi, Japan, Australia na South Korea zatinga Fainali Kombe la Dunia 2010!!!!
Nchi za Uholanzi, Japan, Australia na South Korea jana zimekuwa Nchi za kwanza kufanikiwa kuingia Fainali ya Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwaka 2010.
Japan ndio ilikuwa Nchi ya kwanza kuungana na Mwenyeji Afrika Kusini baada ya kuwafunga Uzbekistan bao 1-0.
Uholanzi, iliyoifunga Iceland 2-1, ikawa ni Timu ya kwanza kutoka Ulaya kuingia Fainali za Kombe la Dunia na South Korea wakicheza Dubai waliwafunga wenyeji wao Nchi ya Falme za Kiarabu [UAE] bao 2-0 na kutinga Fainali.
Australia walibanwa na Wenyeji wao Qatar mjini Doha na kutoka suluhu 0-0 lakini wao walikuwa wakihitaji pointi moja tu ili watinge Fainali.
MATOKEO MECHI NYINGINE ZA KOMBE LA DUNIA:
ZILIZOCHEZWA JANA:

ULAYA:
AZERBAIJAN 0 WALES 1
SLOVAKIA 7 SAN MARINO 0
MARCEDONIA 0 NORWAY O
FINLAND 2 LIECHTENSTEIN 1
BELARUS 5 ANDORRA 1
CYPRUS 2 MONTENEGRO 2
BULGARIA 1 IRELAND 1
SWEDEN 0 DENMARK 1
LITHUANIA 0 ROMANIA 1
CROATIA 2 UKRAINE 2
SERBIA 1 AUSTRIA 0
ALBANIA 1 PORTUGAL 2
AFRIKA:

TUNISIA 2 MOZAMBIQUE 0
MAREKANI YA KUSINI:
URUGAY 0 BRAZIL 4
BOLIVIA 0 VENEZUELA 1
ARGENTINA 1 COLOMBIA 0
PARAGUAY 0 CHILE 2
MAREKANI YA KASKAZINI:
TRINIDAD & TOBAGO 2 COSTA RICA 3
USA 2 HONDURAS 1
EL SALVADOR 2 MEXICO 1
MECHI ZA LEO:
AFRIKA:
CAMEROUN V MOROCCO
BENIN V SUDAN
NIGERIA V KENYA
GUINEA V IVORY COAST
MALI V GHANA
ALGERIA V EGYPT
MAREKANI YA KUSINI:
PERU V ECUADOR
Ferdinand nje Kikosi cha England kitakachocheza Jumatano!!!!
Rio Ferdinand hatakuwemo kwenye Kikosi cha England kitakachocheza na Andorra Jumatano katika mechi ya Kombe la Dunia baada ya kuthibitishwa hajapona misuli ya mguu wake.
Kwa wiki chache sasa Ferdinand amekuwa akisumbuliwa na tatizo hilo na aliachwa kwenye safari ya kwenda Kazakhstan ambapo England walicheza jana na kushinda 4-0 huku iktumainiwa atapona na kucheza Jumatano dhidi ya Andorra.
Katika mechi ya jana, pengo la Ferdinand lilizibwa vizuri na Mathew Upson.
Hull City watoa ofa kwa Chipukizi wa Man U!!!!
Kuna habari kuwa Hull City wametoa ofa ya Pauni Milioni 6 kumnunua Mshambuliaji Chipukizi wa Manchester United Frazier Campbell ambae karibu msimu wote uliokwisha hivi karibuni alikuwa akichezea kwa mkopo Tottenham.
Campbell, 21, mwaka 2007 alichezea kwa mkopo Hull City kwa kipindi cha miezi 7.

No comments:

Powered By Blogger