Saturday 13 June 2009

KOMBE LA MABARA KESHO!!!
Kesho Jumapili, Timu 8 zitaanza kugombea Kombe la Mabara la FIFA, wakati katika mechi ya ufunguzi wenyeji Afrika Kusini watakwaana na Iraq mjini Johannesburg.
Haya ni Mashindano ya 8 ya Kombe hili lililoanza kushindaniwa mwaka 1992.
Washindi wa nyuma ni [Kwenye mabano Nchi ilyokuwa Mwenyeji]:
· 1992: Argentina (Saudi Arabia)
· 1995: Denmark (Saudi Arabia)
· 1997: Brazil (Saudi Arabia)
· 1999: Mexico (Mexico)
· 2001: France (S Korea/Japan)
· 2003: France (France)
· 2005: Brazil (Germany)
Mashindano ya mwaka huu yanashirikisha Nchi 8, Mwenyeji akiwa Afrika Kusini, Italy, Bingwa wa Dunia na Nchi nyingine ni:
-USA: Bingwa wa Nchi za Marekani ya Kaskazini, Kati na Carribean mwaka 2007
-Brazil: Bingwa wa Marekani Kusini mwaka 2007 [Copa America 2007]
-Iraq: Bingwa wa Asia mwaka 2007
-Egypt: Bingwa wa Afrika mwaka 2008
-Spain: Bingwa wa Ulaya mwaka 2008
-New Zealand: Bingwa wa Bara la Baharini [Oceania]
Viwanja:
Miji minne ya Afrika Kusini ndio itakuwa Wenyeji wa mechi za Kombe la Mabara 2009:
-Johannesburg: Kiwanja cha Coca Cola Park [Uwezo Watazamaji 62,567]
-Pretoria: Kiwanja cha Loftus Versfeld [Uwezo Watazamaji 50,000]
-Bloemfontan: Kiwanja cha Free State [Uwezo Watazamaji 48,000]
-Rustenberg: Kiwanja cha Royal Bafokeng [Uwezo Watazamaji 42,000]
Makundi
Timu zimegawanywa kwenye Makundi mawili na:
-KUNDI A: Afrika Kusini, Spain, Iraq na New Zealand
-KUNDI B: USA, Italia, Brazil na Egypt
RATIBA: [saa za bongo]
-Jumapili 14 Juni 2009-06-05
KUNDI A:
Afrika Kusini v Iraq [saa 11 jioni]
New Zealand v Spain [saa 3 na nusu usiku]
-Jumatatu 15 Juni 2009-06-05
KUNDI B
Brazil v Egypt [saa 11 jioni]
USA v Italy [saa 3 na nusu usiku]
-Jumatano 17 Juni 2009-06-05
KUNDI A
Spain v Iraq [saa 11 jioni]
Afrika Kusini v New Zealand [saa 3 na nusu]
-Alhamisi 18 Juni 2009
KUNDI B
USA v Brazil [saa 11 jioni]
Egypt v Italia [saa 3 na nusu usiku]
-Jumamosi 20 Juni 2009
KUNDI A [Mechi zito zinaanza pamoja saa 3 na nusu usiku]
Iraq v New Zealand
Afrika Kusini v Spain
-Jumapili 21 Juni 2009
KUNDI B [Mechi zito zinaanza pamoja saa 3 na nusu usiku]
Italia v Brazil
Egypt v USA
NUSU FAINALI:
Jumatano Juni 24: MSHINDI KUNDI A v MSHINDI WA PILI KUNDI B
Alhamisi Juni 25: MSHINDI KUNDI B v MSHINDI WA PILI KUNDI A
Jumapili 28 Juni: FAINALI

No comments:

Powered By Blogger