Monday 8 June 2009


IMANI ZA NDUMBA ZAHARIBU UWANJA WA KISASA HUKO MBABANE, SWAZILAND!!
Watu wasiojulikana wamekuwa wakiharibu Uwanja wa Taifa wa Somhlolo ulioko Mji Mkuu Mbabane wa Nchi ya Swaziland kwa kufukia vitu usiku wa manane vyenye mwelekeo wa imani za kichawi, au ‘muti’ kama wavyoita huko Swaziland, kwenye eneo la Magoli na kwenye duara la kati la Uwanja huo wa kisasa ambao nyasi zake ni za bandia.
Maafisa wa Michezo wamedai nyasi hizo za bandia ziliwekwa kwa gharama ya Dola za Kimarekani Laki 600 [takriban Shilingi za Bongo 780,000,000]lakini kabla ya mechi kubwa zinazohusu Klabu maarufu hapo Mbabane asubuhi ya siku ya mechi sehemu ya Magoli na duara la kati hukutwa nyasi hizo za bandia zimeunguzwa, kuchimbwa na juju kufukiwa
.

No comments:

Powered By Blogger