Saturday 6 June 2009

Rais wa Real sasa ataka urafiki na Man U!!!!
Rais wa Real Madrid Florentino Perez amedai yeye anajali zaidi urafiki na Manchester United kuliko kumsaini Ronaldo.
Perez amesema: ‘Ikitokea siku moja Ronaldo atakuja kucheza Real basi hiyo itakuwa fahari kwetu! Lakini ikibidi nichague urafiki na Manchester United au kumsaini Ronaldo, ntachagua urafiki na Man U! Na ieleweke sijasema Ronaldo atakuja Bernabeu!’
Perez akaongeza: ‘Ntazungumza na Sir Alex Ferguson na David Gill [Mkurugenzi Mtendaji wa Man U] ili kudumisha urafiki!’’
Wenger-Defensi lazima iimarike!!!
Bosi wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa ana nia ya kuimarisha safu yake ya ulinzi kipindi hiki cha usajili kwani Defensi yao ilikuwa inavuja sana na iliruhusu mabao 37 katika LIGI KUU na wakamaliza nafasi ya 4 kwenye ligi hiyo wakiwa pointi 18 nyuma ya Mabingwa Manchester United.
Kwa sasa Wenger yuko Uchina akisaka Wachezaji na amesema: ‘Msimu ulioisha tulianza ligi pole pole lakini tukaimarika kadri muda ulivyosogea. Tuna Timu changa na itakuwa nzuri tu ingawa inabidi tuimarishe Defensi’

No comments:

Powered By Blogger