Saturday 30 May 2009

KOMBE LA UJERUMANI: Werder Bremen 1 Bayer Leverkusen 0!!!!
Werder Bremen hatimaye wamemaliza msimu wao kwa kishindo kikubwa pale walipolibeba Kombe la Klabu huko Ujerumani baada ya kuwafunga Bayer 04 Leverkusen bao 1-0.
Werder Bremen hivi karibuni walivunjwa mioyo walipofungwa kwenye Fainali ya Kombe la UEFA na Klabu ya Ukraine Shakhtar Donetsk kwa bao 2-1 Fainali hiyo ikiwa ya mwisho kushindaniwa kwa jina la UEFA CUP.
Bao la ushindi la Werder Bremen lilifungwa na Mesut Ozil kwenye dakika ya 58.
Ni furaha kubwa kwa Werder Bremen kwa sababu pia nafasi waliyomalizia Bundesliga isingewaruhusu kucheza Ulaya kama wasingeshinda Kombe hilo.
Msimu ujao kuna mfumo mpya na jina jipya ambalo ni UEFA EUROPA LEAGUE na kwa kuwa wametwaa Kombe hilo la Ujerumani wataingizwa kwenye hiyo UEFA EUROPA LEAGUE.

No comments:

Powered By Blogger