Saturday 30 May 2009

FAINALI: Chelsea v Everton!!!!

Ni Fainali kati ya Meneja Guus Hiddink v Meneja David Moyes!!!

Ni Fainali ya Kombe Kongwe Duniani, Kombe la FA, na hii ni Fainali ya 128 katika historia yake na inazikutanisha Timu mbili zenye Mameneja wenye tofauti kubwa kati yao.
Mameneja hao, Guus Hiddink wa Chelsea na David Moyes wa Everton, leo Uwanjani Wembley, jijini London wataziongoza Timu zao kwenye kimbembe hicho.
Ni watu wawili, ingawa wote ni Mameneja wa Klabu za mpira, walio tofauti kabisa ukichukulia staili zao, uzoefu wao, mbinu zao na hata rasilimali zilizopo kwenye Klabu zao!
Guus Hiddink:
Mafanikio yake: PSV EINDHOVEN [Ubingwa mara 6, Vikombe vingine mara 4, Kombe la Ulaya mara 1] REAL MADRID [Kombe la Mabara (Ubingwa wa Dunia) mara 1]
Guus Hiidink ni Mholanzi anaeamini Soka la Kiholanzi la kupasiana na kucheza kitimu. Yeye ni Balozi mzuri wa Soka Duniani kwani ameshafanya kazi yake pembe nyingi za Dunia.
Ameshafundisha kwao Uholanzi, Spain, Uturuki, Korea ya Kusini, Urusi [ambayo bado ndie Mwajiri wake wa kudumu], Australia na sasa England.
Baada ya mechi ya leo inaaminika Guus Hiddink ataiacha Chelsea na kurudi kwenye kazi yake ya kudumu kama Meneja wa Timu ya Taifa ya Urusi.
Ingawa anaondoka Chelsea, Mashabiki wengi wa Timu hiyo wametokea kumpenda sana kwa jinsi ya ubora wa kazi yake, ucheshi na utu wake. Katika mechi 21 chini yake, Chelsea imefungwa mechi moja tu!
David Moyes, Meneja wa Everton kuanzia 2002:
Mafaniko yake: PRESTON NORTH END [Iliyokuwa Daraja la 2 sasa linaitwa LIGI WANI, Mabingwa 1999-2000] EVERTON [Hajashinda Kombe lolote ila yeye binafsi amepewa Tuzo ya Meneja Bora wa LIGI KUU kwa miaka mitatu mfululizo hadi sasa]
Tangu ajiunge Everton mwaka 2002, hajashinda Kikombe chochote lakini amefanikiwa kuiinua Klabu isiyo na utajiri mkubwa na kuiwezesha kuwa miongoni mwa Klabu 6 Bora za LIGI KUU.
Kwa mafaniko hayo, ndio maana Mameneja wenzake kwenye Chama chao cha Mameneja [LMA=League Managers Association] kimemtunuku Tuzo ya Meneja Bora kwa misimu mitatu mfululizo sasa.
Msimu huu, David Moyes ameiwezesha Everton kutoka sare ya 0-0 na Chelsea katika mechi zote mbili za LIGI KUU England na pia kuifanya Everton ishike nafasi ya 5 kwenye ligi hiyo na hivyo kucheza Ulaya kwenye Mashindano mapya msimu ujao yatakayoitwa UEFA EUROPA LEAGUE .

No comments:

Powered By Blogger