Sunday 24 May 2009

LEO NI LEO: KUZAMA AU KUZUKA!!!
Ni WAWILI gani kati ya Sunderland, Hull City, Newcastle na Middlesbrough kuungana na West Brom kushuka DARAJA???
Tamati ya LIGI KUU England ni leo jioni wakati Timu zote 20 zitashuka Viwanja mbalimbali kucheza mechi zao za mwisho kuanzia saa 12 jioni saa za kibongo huku tayari Bingwa Manchester United alitawazwa tangu wiki iliyopita na kuacha kimbembe kikubwa cha Timu zipi mbili zitaungana na West Bromwich Albion kucheza ‘mchangani’ Ligi ya chini iitwayo Coca Cola Championship msimu ujao.
Ingawa macho ya wengi yako kwenye ‘VITA KUU’ ya nani atashushwa Daraja lakini kimahesabu hata nafasi za pili na za tatu zinaweza kugeuka ikiwa leo Liverpool, alie nafasi ya 2, akifungwa na Tottenham na Chelsea, alie nafasi ya 3, akamfunga Sunderland mabao mengi ili kuifuta tofauti ya magoli bora ya Liverpool ya magoli matano aliyokuwa nayo.
Nafasi ya 4 ni ya Arsenal na hakuna anaeweza kumpiku.
Kwa kumaliza nafasi 3 za juu, Timu za Manchester United, Liverpool na Chelsea zinaingia moja kwa moja kwenye hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao.
Arsenal, kwa kumaliza nafasi ya 4, pia anaingia UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao lakini itabidi aanzie Raundi ya Mwanzo ya Mtoano na hatari ya mfumo wa msimu ujao ni kuwa anaweza kupangiwa Timu yeyote ile tofauti na misimu ya nyuma ambapo Timu Bora zilitenganishwa.
Ingawa Sunderland wako nafasi ya 16 wakiwa na pointi 36 lakini wakifungwa watashushwa ikiwa Newcastle na Hull City watashinda.Ikiwa Newcastle watashinda na Hull City kutoka droo basi Sunderland [IKIWA HATOFUNGWA ZAIDI YA BAO 5] na Newcastle watapona na badala yake Hull City wataporomoka.
Middlesbrough ndie anayeomba maajabu yatokee!!
Ili Middlesbrough apone itabidi kwanza ashinde mechi yake na kuomba Hull City na Newcastle wafungwe lakini nani atashushwa kati ya Middlesbrough na Hull City itategemea Middlesbrough kafunga bao ngapi na Hull City kafungwa ngapi.
Hizo, kwa ufupi, ndizo hesabu kali za nani atasalimika kubaki LIGI KUU.
Msimamo kwa Timu za chini zilizo kwenye VITA KUU ya KUJINUSURU KUSHUSHWA DARAJA ni [West Bromwich tayari kaporomoka]: [TIMU ZA NAFASI YA 18 HADI 20 HUSHUSHWA]

-Nafasi ya 16: Sunderland pointi 36 [tofauti ya magoli -19]
-Nafasi ya 17: Hull City pointi 35 [tofauti ya magoli -24]
-Nafasi ya 18: Newcastle pointi 34 [tofauti ya magoli -18]
-Nafasi ya 19: Middlesbrough pointi 32 [tofauti ya magoli -28]
-Nafasi ya 20: West Brom pointi 31 [tofauti ya magoli -31]
MECHI ZA MOTO ZA TIMU ZA CHINI:
Aston Villa v Newcastle
Hull v Man U
Sunderland v Chelsea
West Ham v Middlesbrough
RATIBA KAMILI:
Jumapili, 24 Mei 2009
[saa 12 jioni]
Arsenal v Stoke
Aston Villa v Newcastle
Blackburn v West Brom
Fulham v Everton
Hull v Man U
Liverpool v Tottenham
Man City v Bolton
Sunderland v Chelsea
West Ham v Middlesbrough
Wigan v Portsmouth
KASKAZINI MASHARIKI YA ENGLAND YAGUBIKWA NA MAJONZI!!!!
· Ni woga wa Timu za Mijini kwao KUSHUSHWA DARAJA!!!!
· Ni miji ya Hull, Middlesbrough, Sunderland na Newcastle!!!!
Wiki yote iliyopita Dereva mmoja wa Basi la Abiria linalofanya safari kati ya miji iliyoko Kaskazini Mashariki ya England, miji ya Hull, Middlesbrough, Sunderland na Newcastle, ambayo yote iko eneo moja lakini kwa bahati mbaya, imeunganishwa katika VITA KUBWA ya kunusuru Klabu zao kuporomoka kutoka LIGI KUU England, amekuwa akifanya kazi yake kama kawaida lakini kitu pekee anachokisikia wiki nzima miongoni mwa abiria wanaosafiri kwenye basi lake ni huzuni, matumaini na stori nyingi kuhusu Klabu za Hull City, Middlesbrough, Sunderland na Newcastle.
Safari yake kila asubuhi huanzia Hull na kuelekea kaskazini kwenda Middlesbrough halafu Sunderland na kumalizikia Newcastle.
‘Ni majonzi na masikitiko eneo lote!’ Dereva huyo anasema. ‘Binafsi nafikiria Hull City watashushwa pamoja na Middlesbrough hata kama Man U wataleta Kikosi cha pili Hull hawezi kuwafunga!! Nadhani Newcastle atapata pointi yake moja anusurike!’
Kila kona ya Miji hiyo minne, gumzo ni nani atapona?
Homa hii ya kunusuru Klabu zao imeingia mpaka ndani ya Klabu zenyewe na Gazeti moja la mjini Hull limeripoti Klabu ya Hull imempiga marufuku Shabiki wake mmoja mwenye tiketi ya msimu mzima kuingia KC Stadium kutoingia uwanjani humo baada ya kugundulika anatoa matusi mengi Timu yake Hull City inapocheza.
Lakini nani amlaumu Shabiki huyo ikiwa Hull City katika mechi 10 za mwisho ilizocheza uwanjani kwake KC Stadium haijashinda hata mechi moja??
Hilo ndilo kasheshe lililoikumba Miji ya Kaskazini Mashariki ya England!!!!

No comments:

Powered By Blogger