Friday 29 May 2009

FAINALI: CHELSEA v EVERTON
Wembley Stadium, London Jumamosi 30 Mei 2009 saa 11 jioni [bongo taimu]
Timu za LIGI KUU England Chelsea na Everton zinakutana Fainali ya Kombe la FA hapo kesho Jumamosi 30 Mei 2009 uwanjani Wembley.
Mbali ya kunyakua Kombe hilo ambalo ndilo linalosemekana ni la zamani sana kuanzwa kushindaniwa kwenye soka Duniani kupita Kombe lolote lile, mshindi ataibuka na kitika cha fedha Pauni Milioni 2 taslimu na atakaeshindwa atapata Pauni Milioni moja.
Mara ya mwisho kwa Everton kucheza Fainali ilikuwa mwaka 1995 walipoifunga Manchester United 1-0 na kuchukua Kombe hilo.
Chelsea nao wa walicheza Fainali mara ya mwisho mwaka 2007 na pia kuifunga Manchester United 1-0 na kunyakua Kombe hilo.
Hii itakuwa ni Fainali ya 128 ya FA Cup na ni mara ya 75 kuchezewa Uwanja wa Wembley.
Msimu huu jumla ya mechi 925 zilichezwa kushindaniwa Kombe hili na jumla ya magoli 3035 yalifungwa. Mechi iliyotoa magoli mengi ni ile ya Mildenhall Town 8 Felixstowe & Walton United 0.
Fainali ya kesho ya Chelsea v Everton ni ya 20 kwa Timu hizi mbili na Chelsea amechukua Kombe mara 4 na Everton mara 5.
Mbele ya Mashabiki 90,000, Chelsea watashuka uwanjani wakiwa na jezi za njano mwili mzima na Everton watakuwa na uzi wao ule ule wa kawaida wa kibuluu, bukta nyeupe na stokingi nyeupe.
Chelsea msimu huu wamemaliza nafasi ya 3 na Everton nafasi ya 5 kwenye LIGI KUU.
Vikosi vinategemewa:
Chelsea [Mfumo, pengine 4-3-3]: Cech, Bosingwa, Alex, Terry, A. Cole, Essien, Mikel, Lampard, Malouda, Drogba, Anelka.
Everton [Mfumo, pengine 4-4-1-1]: Howard, Hibbert, Yobo, Lescott, Baines, Osman, Neville, Cahill, Pienaar, Fellaini, Saha.
Refa: Howard Webb

No comments:

Powered By Blogger