Monday 25 May 2009

Wolves, Birmingham na Sheffield United AU Burnley kuchukua nafasi za Newcastle, Middlesbrough na West Brom LIGI KUU msimu ujao!!!

==LEO ITAJULIKANA NI SHEFFIELD UNITED AU BURNLEY!!!
Leo saa 11 jioni bongo taimu Timu mbili za Daraja la Coca Cola Championship, Burnley na Sheffield United, zitapigana ndani ya Uwanja wa Wembley, jijini London kutafuta Timu moja ipi itaungana na Wolverhamton Wanderers, aliemaliza Ligi hiyo nafasi ya kwanza, na Birmingham, aliemaliza wa pili, kucheza LIGI KUU England msimu ujao.
Sheffield United na Burnley zilishinda mechi zao za awali za Mtoano kwa Sheffield United kuwatoa Preston kwa jumla ya mabao 2-1 katika mechi mbili na Burnley waliwanyuka Reading jumla ya bao 3-0 katika mechi mbili.
Katika mfumo wa Ligi ya Coca Cola Championship Timu mbili za kwanza huingia LIGI KUU moja kwa moja na Timu zilizo nafasi ya 3 hadi ya 6 hucheza Mtoano maalum ili kupata Timu moja itakayoungana na hizo Timu mbili za kwanza kupanda kwenda LIGI KUU.
Katika mechi mbili za Ligi, Burnley ilshinda mechi zote kwa kuifunga Sheffield United nyumbani kwake mabao 3-2 katika mechi ya kwanza na marudiano yalikuwa nyumbani kwa Burnley na walishinda tena bao 1-0.
Mbali ya umuhimu wa kupanda Daraja kwenda LIGI KUU, Timu zinazokuwa LIGI KUU hunufaika kwa kuingiza pesa nyingi sana na ndio maana mechi hii imebatizwa jina la 'MECHI MOJA YA KLABU YENYE THAMANI SANA DUNIANI!!' kwa vile mshindi akichezea LIGI KUU ataingiza MAPATO YA WASTANI wa zaidi ya Pauni Milioni 60 kwa msimu!!
Burnley mara ya mwisho kuchezea Darala la juu kabisa ilikuwa miaka 33 iliyopita na mwaka huu wana matumaini makubwa sana ya kufaulu kupanda hasa baada ya kuzitoa Timu za LIGI KUU kwenye Carling Cup msimu huu kama vile Arsenal, Chelsea na West Brom lakini wakatolewa Nusu Fainali na Tottenham ingawa walishinda mechi ya kwanza ya Nusu Fainali hiyo.
Sheffield United waliporomoshwa toka LIGI KUU misimu miwili iliyopita katika mechi ya mwisho katika lile sakata maarufu la Carlos Tevez kuichezea West Ham na kuiokoa West Ham kushushwa kwa kuifungia bao walipocheza na Manchester United mechi ya mwisho ya Ligi.
Refa katika mechi ya leo ni Mike Dean.

No comments:

Powered By Blogger