Thursday 28 May 2009

MBINU HAZIKUWA NZURI-MAN U WAKUBALI!

Baada ya kuchapwa 2-0 na kupokonywa Kombe la Klabu Bingwa la Ulaya na Barcelona, Manchester United wamekekubali kabisa mbinu zao zilikuwa ovyo na Timu haikucheza kabisa kwenye kiwango kinachotakiwa. Meneja wao Sir Alex Ferguason alisema: 'Messi hakuwa tatizo! Xavi na Iniesta walimiliki mpira usiku mzima! Hatukucheza vizuri hata kidogo!' Ronaldo nae alikubali: 'Huu ndio mpira. Mnashinda ua kufungwa! Wao walicheza vizuri lakini sisi mbinu zetu hazikuwa nzuri!' Ferdinand: 'Lazima uwasifie Barcelona! Wamecheza vizuri sana!' Kipa Edwin van der Sar nae alisema: 'Lile goli la kwanza liliwapa imani na wakaanza kucheza mpira wao wa kawaida! Tumefungwa! Msimu ujao inabidi turudi upya na sisi tuna uwezo huo!'


No comments:

Powered By Blogger