Saturday 30 May 2009

Chelsea wachukua FA CUP: Chelsea 2 Everton 1
Licha ya kufunga goli mapema mno na kuvunja ile rekodi ya Fainali ya FA Cup iliyowekwa mwaka 1895 na Mchezaji wa Aston Villa Bob Chatt aliefunga sekunde 30 tangu mechi ianze, Luis Saha aliifungia Everton bao sekunde 25 tu tangu mechi ianze lakini Chelsea waliibuka na kuitawala Fainali hii ya Kombe la FA na mwishowe kuwa washindi wa bao 2-1.
Rekodi nyingine iliyowekwa leo ni ile ya Ashley Cole kuweza kushinda Kombe la FA mara 5 na kuwapita Ryan Giggs, Roy Keane, Mark Hughes, David Seaman na Ray Parlour wote waliochukua Kombe hilo mara 4.
Wengine walioweza kushinda Kombe hili la FA mara 5 ni Charles Wollaston, Arthur Kinnaird na Jimmy Forrest lakini hawa wote waliweka rekodi hii Karne ya 19!!!
Ashley Cole alishinda Kombe lake la kwanza akiwa na Arsenal walipowafunga Chelsea 2002 na kulitetea tena dhidi ya Southampton msimu uliofuata. Mwaka 2005 alishinda tena kwa matuta dhidi ya Manchester United na akahamia Chelsea na kuwafunga Man U 1-0 na leo ni kichwa cha Everton.
Chelsea walisawazisha bao lao kupitia Didier Drogba dakika ya 20 na mpaka mapumziko gemu ilikuwa 1-1.
Ndipo Frank Lampard alipoachia mkwaju nje ya boksi dakika ya 71 na kuwapa Chelsea Kombe la FA.
VIKOSI:
Chelsea: Cech, Bosingwa, Alex, Terry, Ashley Cole, Essien, Mikel, Lampard, Anelka, Drogba, Malouda. Akiba: Hilario, Ivanovic, Di Santo, Ballack, Kalou, Belletti, Mancienne.

Everton: Howard, Hibbert, Yobo, Lescott, Baines, Osman, Neville, Pienaar, Cahill, Fellaini, Saha. Akiba: Nash, Castillo, Vaughan, Jacobsen, Rodwell, Gosling, Baxter.

No comments:

Powered By Blogger