Sunday 24 May 2009

NEWCASTLE, MIDDLESBROUGH WAUNGANA NA WEST BROM KUSHUKA DARAJA!!!
  • TIMU ZOTE ZILIZOKUWA ZIKIPIGANIA KUTOSHUKA DARAJA ZAFUNGWA LAKINI HULL CITY NA SUNDERLAND WANUSURIKA!!!!!!!

Timu zote zilizokuwa kwenye VITA KUU ya kuepuka kushuka Daraja zimefungwa katika mechi zao za mwisho za LIGI KUU England leo lakini ni Newcastle na Middlesbrough ndio walioungana na West Bromwich Albion kushushwa Daraja na msimu ujao watacheza Daraja la chini liitwalo Coca Cola Championship.

MATOKEO YA MECHI YA TIMU ZILIZOKUWA ZIKIPIGANIA KUPONA KUSHUSHWA NI:

Sunderland 2 Chelsea 3

Hull City 0 Manchester United 1

Aston Villa 1 Newcastle 0

West Ham 2 Middlesbrough 1

BAADA YA MECHI ZA MWISHO ZA LEO MSIMAMO KWA TIMU ZA CHINI NI:

[TIMU ZA NAFASI YA 18 HADI 20 HUSHUSHWA]

-Nafasi ya 16: Sunderland pointi 36

-Nafasi ya 17: Hull City pointi 35

-Nafasi ya 18: Newcastle pointi 34

-Nafasi ya 19: Middlesbrough pointi 32

-Nafasi ya 20: West Brom pointi 31

MATOKEO KAMILI MECHI ZA LEO:

Arsenal 4 v Stoke 1

Aston Villa 1 v Newcastle 0

Blackburn 0 v West Brom 0

Fulham 0 v Everton 2

Hull 0 v Man U 1

Liverpool 3 v Tottenham 1

Man City 1 v Bolton 0

Sunderland 2 v Chelsea 3

West Ham 2 v Middlesbrough 1

Wigan 1 v Portsmouth 0

No comments:

Powered By Blogger