Saturday 30 May 2009

ATHARI NA HATARI YA ARSENAL KUSHIKA NAFASI YA 4 LIGI KUU!!!
Kwa kumaliza katika nafasi ya 4 katika msimamo wa LIGI KUU England, Arsenal wamefanikiwa kupata nafasi ya kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao pamoja na Bingwa Manchester United, Mshindi wa pili Liverpool na Chelsea alieshika nafasi ya 3.
Lakini, wakati Manchester United, Liverpool na Chelsea wataingia kwenye hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE, Arsenal inabidi aanze kwenye hatua ya Mtoano.
Katika misimu mitatu iliyopita, Arsenal ilimudu kukipita kikwazo hiki cha kucheza hatua ya Mtoano na kuingia hatua ya Makundi kwa kufaulu katika mechi za nyumbani na ugenini dhidi ya FC Twente, Sparta Prague na Dynamo Zagreb.
Lakini msimu ujao kuna hatari kubwa ya Arsenal kuteleza kwani UEFA wameubadilisha mfumo wa nani unaweza kukutana nae kwenye hatua hiyo ya awali ya Mtoano. Mfumo huu mpya unatoa uwezo mkubwa Arsenal kukutanishwa na Timu ‘kigogo’ ambayo kama Arsenal ilimaliza ligi ya kwao nafasi ya chini kidogo.
Mfumo huu, ulioshabikiwa sana na Rais wa UEFA, Michel Platini, una lengo la kuzisaidia zile Nchi ‘ndogo’ na ‘hafifu’ huko Ulaya ili ziweze kuingia hatua ya Makundi.
Mfumo huu mpya unaifanya Arsenal kuingizwa kwenya kapu moja pamoja na Timu zilizomaliza nafasi ya 4 huko Italy na Spain pamoja na Timu zilizomaliza nafasi ya 3 huko Ujerumani na Ufaransa. Hizi ni Nchi 5 zilizopewa upendeleo maalum wa kutoanza hatua ya awali kabisa ya Mtoano.
Timu zitakazoanza hatua ya awali kabisa ya Mtoano ni zile Timu zinazotoka Nchi 10 zilizoshika nafasi ya 2 kutoka Ureno, Uholanzi, Scotland, Turkey, Ukraine, Belgium, Greece, Czech Republic, na Romania pamoja na Timu ya 3 kutoka Urusi na zitapigiwa dro maalum ili kuzigawa katika mechi 5 zitakazochezwa nyumbani na ugenini kupata Washindi watano.
Washindi watano kutoka kundi la Nchi hizo 10 watajumuika na lile la kundi la Arsenal [yaani Timu kutoka England, Italy, Spain, Ujerumani na Ufaransa] kufanya jumla ya Timu 10 ambazo zitagawanywa Timu Bora 5 kapu moja na Timu ‘sio bora’ kapu jingine na itapigwa kura kupata nani kutoka Kapu Bora anacheza na Timu ipi kutoka Kapu la pili kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na Washindi hao watano wataingizwa kwenye hatua ya Makundi.
Ingawa Arsenal, kufuatia rekodi yake nzuri ya miaka ya hivi karibuni kwenye Mashindano ya UEFA, ana hakika ya kuwekwa Kapu la Timu Bora lakini hata hizo Timu zitazokuwa Kapu la pili hazitakuwa Timu dhaifu na hii ndio athari na hatari kubwa inayoweza kumkuta Arsenal kwa kumaliza nafasi ya 4 kwenye
LIGI KUU England.

No comments:

Powered By Blogger