Sunday 24 May 2009

SCOTLAND: Rangers wachukua Ubingwa wa LIGI KUU Scotland!!
Kwa mara ya kwanza tangu 2005 leo Rangers wamenyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya Scotland baada ya kuwafunga Dundee United mabao 3-0 katika mechi ya mwisho ya msimu na hivyo kuwabwaga Wapinzani wao wa Jadi Celtic katika kinyang'anyiro hicho.
Celtic wamekuwa Mabingwa wa Scotland mara 3 mfululizo tangu mwaka 2006 na hata leo kama Rangers wangeteleza na wao Celtic kushinda basi wangeweza kuutwaa tena.
Hata hivyo Celtic katika mechi yao ya mwisho ya leo wameambulia sare ya 0-0 na Hearts.

No comments:

Powered By Blogger