Monday 25 May 2009

Baada ya Balaa la kushushwa Daraja.......Shearer akataa kuthibitisha kama atabaki Newcastle

................Southgate ategemea Wachezaji kuikimbia Middlesbrough!!

==Baada ya kupona Balaa la kushushwa Daraja Sbragia wa Sunderland abwaga manyanga!!!!
Meneja wa Newcastle, Alan Shearer, baada ya Timu yake kushushwa Daraja walipofungwa na Aston Villa hapo jana, amekataa kujibu maswali yeyote kuhusu nini hatima yake.
Shearer alijibu maswali hayo kwa kusema: 'Ntakutana na Mmiliki wa Klabu wiki hii na ntamwambia nin kilienda sawa na nini kilienda vibaya lakini sasa si wakati wa kusema nini cha baadae!!'
Mwenzake wa Middlesbrough, Gareth Southgate, amekiri kuwa kutakuwa na wimbi la Wachezaji watakaohama kwa vile hawataki kucheza Daraja la chini.
'Bila shaka kutakuwa na mabadiliko makubwa kwa Wachezaji,' Southgate alisema. 'Watu watakuwa na ajenda binafsi! Kama Klabu itabidi tuuze Wachezaji ili tupate pesa za kusonga mbele. Na inabidi tubadilishe hali.'
Na katika hali ya kushangaza, ingawa Sunderland ilinusurika kuporomoka Daraja ingawa ilifungwa na Chelsea mabao 3-2, Meneja wake Ricky Sbragia, mara baada ya mechi, alitangaza kujiuzulu.
Sbragia alitamka: 'Nahisi Klabu inabidi imlete Meneja mwenye jina kubwa!! Niliichukua Klabu hii wakati mgumu sana!!!'
Sbragia aliteuliwa kuwa Meneja mwezi Desemba 2008 mara tu baada ya Roy Keane kubwaga manyanga mwenyewe bila kutegemewa.

No comments:

Powered By Blogger