Saturday 30 May 2009

VETERANI NA SUPASTAA WA URENO FIGO KUSTAAFU SOKA KESHO!!!
Kiungo Luis Figo ametangaza rasmi kustaafu Soka kesho wakati Klabu yake Inter Milan, ambao ndio Mabingwa wa Italia, itakapokuwa nyumbani San Siro kucheza na Atalanta katika mechi ya mwisho ya msimu wa Serie A huku tayari Inter Milan washauchukua Ubingwa.
Figo alijiunga na Inter Milan mwaka 2005 na ameisaidia Klabu hiyo kunyakua Ubingwa wa Italia kwa mara 4 mfululizo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 ambae mwaka 2001 ndie alikuwa Mchezaji Bora Duniani alijitengenezea jina lake alipozichezea Barcelona na Real Madrid za Spain.
Figo alihama Barcelona na kwenda Real Madrid mwaka 2000 na mwaka 2002 alichukua Klabu Bingwa Ulaya akiwa na Real.
Katika mechi yake ya kwanza kurudi uwanjani Nou Camp akiichezea Real Madrid tangu ahame Barcelona, Mashabiki wa Barcelona walimrushia kichwa cha nguruwe.
Figo ndie Mchezaji anaeshikilia rekodi ya kuchezea Timu ya Taifa ya Ureno mechi nyingi kwa kucheza mechi 127 na kufunga magoli 32.

No comments:

Powered By Blogger