Saturday 30 May 2009

Paolo Maldini kustaafu kesho!!!!

Kesho kwenye mechi ya SERIE A huko Italia kati ya wenyeji ACF Fiorentina na AC Milan, Nahodha wa AC Milan Paolo Maldini mwenye umri wa miaka 40 ataingia uwanjani akiwa amevaa Jezi yake Namba 3 kwa mara ya mwisho kwa vile yeye mwenyewe, baada ya kucheza misimu 25, anastaafu na kwa heshima na kumtukuza yeye binafsi Klabu ya AC milan imeamua Jezi Namba 3 nayo istaafishwe.
Katika kipindi cha miaka 25, Nahodha Paolo Maldini ambae pia alichezea Timu ya Taifa ya Italia na kuwa Nahodha pia, amefaulu kuchukua Vikombe 26 ikiwa pamoja na vile vya Klabu Bingwa Ulaya mara 5.
Ingawa kesho ni mechi yake ya mwisho, Paolo Maldini hataki kutoka uwanjani kwa kufungwa na Fiorentina kwani kufungwa kutamaanisha Fiorentina wanaipiku AC Milan na kutwaa nafasi ya 3 msimamo wa Ligi SERIE A na hivyo kucheza moja kwa moja hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao.
Paolo Maldini, kama Baba yake mzazi Cesare Maldini, ndio Manahodha wa muda mrefu wa AC Milan na hata Baba yake aliwahi kulibeba Kombe la Klabu Bingwa Ulaya.
Mwenyewe Paolo Maldini anamsifia Nahodha wa AC Milan aliemrithi aliekuwa akiitwa Franco Baresi na kumsema huyo ndie alikuwa akimpa motisha kubwa sana.
Baresi ni mmoja wa Wachezaji wa Italia wenye jina kubwa na sifa kubwa.
Paolo Maldini anasema anakumbuka na kuyakumbuka matukio mawili na kuyaona ni bora maishani mwake ambayo ni pale mwaka 2003 katika Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE walipowabwaga Wapinzani wao wa Italia Juventus kwa matuta ya mabao 3-2 baada ya kutoka suluhu 0-0.
Lakini siku spesho moyoni mwake ni Mei 2001 walipowakung'uta Wapinzani wao wa Jadi FC Internazionale Milano, maarufu kama Inter Milan, mabao 6-0!!!
Paolo Maldini anasema: 'Hiyo ilikuwa spesho kwa Familia yangu!!! Baba yangu Mzazi ndie alikuwa akiongoza Benchi la AC Milan!!'
Kwa sasa Paolo Maldini anaishi kwa matumaini makubwa kuwa Mwanawe Christian Maldini anaechezea Timu ya Vijana ya AC Milan atafuata nyayo za Baba na Babu yake!!!
Pengine, hapo, ndipo Jezi Nambari 3 itatoka kwenye kustaafu na kurudi uwanjani!!!!
Steven Gerrard: 'Tukipata Wachezaji Wawili au Watatu tutawafikia Man U!!!!'
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, ametamka kuwa Liverpool ina upungufu wa Wachezaji Wawili au Watatu wazuri ili kufikia kiwango cha Mabingwa Manchester United.
Gerrard, alieiongoza Liverpool kushika nafasi ya pili LIGI KUU England na pia kufikia Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu huu, anaamini Meneja wake Rafa Benitez ameweka mkakati wa kuziba upungufu huo.
Gerrard anasema: 'Nina hakika Rafa anashughulikia mapungufu! Ni muhimu kuziba kwani ukitazama Mabenchi ya Akiba ya Man U na Chelsea utashangaa kuona Wachezaji Mastaa na Bora sana hawachezi!'
Gerrard akaongeza: 'Tumecheza vyema msimu huu! Tumemaliza tukiwa na pointi 86 na mara nyingi pointi hizi zinakupa Ubingwa!! Lakini pongezi kubwa kwa Man U!!!!'

No comments:

Powered By Blogger