Wednesday 27 May 2009

Anderson aahidi kukimbia uchi akifunga goli!!!
Chipukizi wa Brazil, Anderson, ameahidi atavua jezi na kukimbia uchi akifunga goli kwenye Fainali ya leo kati ya Klabu yake Manchester United na Barcelona itakayochezwa Stadio Olimpico kugombea UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Anderson hajawahi kufunga bao kwenye mechi yeyote ya Manchester United na mpaka sasa ameshacheza mechi 73 tangu ajiunge kutoka FC Porto mwaka 2007.
Goli pekee alilofunga ni lile la penalti katika Fainali ya msimu uliopita ambayo Man U waliwabwaga Chelsea kwa mikwaju ya penalti tano tano na kutwaa Kombe la UEFA CHAMPIONS LEAGUE huko Moscow, Urusi.
Shabiki wa Man U achomwa kisu huko Roma!!! Wengine wawili wakamatwa!!!
Vibweka vya Fainali ya leo huko Roma, Italia kati ya Mabingwa Watetezi Manchester United na Barcelona vimeanza kupamba moto baada ya taarifa kupatikana kuwa Shabiki mmoja wa Man U, Greg Wheldon, 34, amechomwa visu mapajani na matakoni nje ya hoteli yake iliyo karibu na Vatican.

Genge la Wahuni wa huko Italia lijulikanalo kama 'Ultras' ndio wanaaminika wamefanya unyama huo kwani wana staili ya kuchoma watu visu mapajani na matakoni.
Shabiki huyo alipelekwa hospitali alfajiri ya leo na kuruhusiwa kutoka baadae na Msemaji wa Hospitali iliyomtibu amesema majeraha yake si ya ‘kutisha’.
Maelfu ya Mashabiki wa Manchester United wameivamia Roma kushuhudia Fainali ya leo.
Wakati huo huo, Msemaji wa Polisi, Marcello Cardona, amethibitisha kuwa Mashabiki wawili wa Man U ambao ni Baba na Mwanawe wako lupango baaada ya kuwa njwii na kuwashambulia wapita njia katika eneo la Campo de Fiori ambalo linapendwa na Watalii.
Uuzwaji wa pombe jirani na Stadio Olimpico umepigwa marufuku kuanzia jana jioni hadi kesho asubuhi.

BUTI ZA ROONEY ZAIBIWA!!!!!
Buti za kuchezea soka za Wayne Rooney wa Manchester United zilizosafirishwa kwa ndege na Kampuni ya Nike hadi Roma, Italia zimeibiwa baada ya kupokelewa Uwanja wa Ndege huko Roma.
Inasemekana kuna mtu alisaini kuzipokea buti hizo spesheli aina ya Nike T90 na baada ya hapo zikatoweka.
Kwa sasa, Nike wanahaha kumtumia buti nyingine ili ziwahi mechi ya leo.
Wigan yairuhusu Sunderland kuongea na Meneja Steve Bruce!
Klabu ya Sunderland imepewa idhini na Wigan kufungua majadiliano ya kumchukua Meneja wa Wigan Steve Bruce.
Sunderland kwa sasa haina Meneja baada ya Meneja wao Ricky Sbragia kuitema Klabu mara tu baada ya Sunderland kunusurika kuteremshwa daraja siku ya Jumapili licha ya kufungwa na Chelsea 3-2.

Timu zilizoshuka ni Newcastle, Middlesbrough na West Brom.
Sbragia alirithi cheo hicho Desemba 2008 baada ya Roy Keane kubwaga manyanga mwenyewe.
Ferguson, Vidic ndio Meneja na Mchezaji Bora wa LIGI KUU England msimu huu 08/09!!!!

Mwanawe Ferguson, Darren, atwaa Umeneja Bora LIGI WANI!!
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, na Mchezaji wake, Nemanja Vidic, wamepewa Tuzo ya Meneja Bora
na Mchezaji Bora wa LIGI KUU England msimu huu wa mwaka 2008/9.
Vilevile mtoto wake Ferguson aitwae Darren Ferguson, ambae ni Meneja wa Peterborough Timu iliyokuwa Daraja liitwalo LIGI WANI [LEAGUE 1] ameshinda Tuzo ya Meneja Bora kwa Daraja hilo baada ya kuweza kuipandisha Peterborough hadi Daraja la juu Coca Cola Championship.
LIGI WANI ni Daraja la chini ya Coca Cola Championship ambayo ipo chini ya LIGI KUU.
Ferguson na Vidic wamepewa Tuzo hizo kwa kutambua mchango wao mkubwa msimu huu ulioiwezesha Manchester United kutwaa Ubingwa wa LIGI KUU kwa mara ya 3 mfululizo.
Hii ni mara ya 9 kwa Ferguson kushinda Tuzo hii na ni mara ya kwanza kwa Vidic.
Jopo la Wawakilishi kutoka FA, Vyombo vya Habari na Mashabiki ndio waliotoa uamuzi wa kuwazawadia Ferguson na Vidic.
Meneja Mkuu Bayern atoboa Man U imewauliza kuhusu Ribery!!!
Meneja Mkuu wa Klabu ya Bayern Munich, Uli Hoeness, ametoboa kuwa Manchester United imewafuata kuulizia kuhusu Mchezaji wao Franck Ribery wa Ufaransa.
Inaaminika mbali ya Man U, Klabu kubwa kadhaa za Ulaya zinamuwania Ribery ambae bado ana miaka miwili kwenye mkataba wake na Bayern Munich. Miongoni mwa Klabu hizo ni Barcelona na Real Madrid.

No comments:

Powered By Blogger