Monday 25 May 2009

Burnley watua LIGI KUU England!!!!! Waitungua Sheffield United 1-0!!!
BURNLEY, WOLVES NA BIRMINGHAM KUZIBADILI NEWCASTLE, MIDDLESBROUGH NA WEST BROM LIGI KUU MSIMU UJAO!!!!

Baada ya miaka 33 ya kutokucheza Daraja la juu kabisa la Soka huko England, leo huko Wembley Stadium, London, Timu ya Burnley imeifunga Sheffield United bao 1-0 na kufanikiwa kuingia LIGI KUU.
Goli lililoipeleka Burnley LIGI KUU lilifungwa na Wade Elliot dakika ya 13.
Hii ilikuwa ni Fainali ya Mtoano maalum wa kuipata Timu ya tatu itayoungana na Wolves na Birmingham zilizoingia moja kwa moja LIGI KUU kwa kuwa zilimaliza Ligi ya Coca Cola Championship nafasi za kwanza na ya pili.
Timu za Wolves, Birmingham na Burnley zinapanda Daraja kwenda LIGI KUU kuchukua nafasi za Newcastle, Middlesbrough na West Bromwich Albion zilizoshushwa na sasa zitacheza Coca Cola Championship msimu ujao.
Veterani Neville aitwa tena Timu ya Taifa England!!!!
Meneja wa England, Fabio Capello, katika hatua ya kushangaza amemuita kwenye Kikosi cha England Nahodha wa Manchester United Gary Neville [34] kwa ajili ya mechi za mchujo wa kuingia Fainali za Kombe la Dunia ambazo England itacheza na Kazakhstan Juni 6 na siku nne baadae watacheza na Andorra.
Gary Neville, ambae mara ya mwisho alichezea England Oktoba 2007 wakati England ilipofungwa na Urusi kwenye mchujo wa kuingia EURO 2008, amekuwa akiandamwa na kuumia mara kwa mara na kuifanya hata namba yake Klabuni kwake Manchester United isiwe ya kudumu.
Pia, Capello amemchukua tena aliyekuwa Kipa nambari wani wa England, Paul Robinson wa Blackburn baada ya Makipa wa sasa Nambari moja na mbili, David James wa Portsmouth na Ben Foster wa Manchester United kuumia. Robinson atasaidiwa na Makipa Scott Carson wa West Brom na Robert Green wa West Ham.
Kikosi kamili na Klabu wanazotoka ni kama ifuatavyo:
Scott Carson (West Bromwich Albion), Robert Green (West Ham United), Paul Robinson (Blackburn Rovers)
Wayne Bridge (Manchester City), Ashley Cole (Chelsea), Rio Ferdinand (Manchester United), Glen Johnson (Portsmouth), Joleon Lescott (Everton), Gary Neville (Manchester United), John Terry (Chelsea), Matthew Upson (West Ham United)
Gareth Barry (Aston Villa), David Beckham (AC Milan mkopo kutoka LA Galaxy), Michael Carrick (Manchester United), Steven Gerrard (Liverpool), Frank Lampard (Chelsea), Theo Walcott (Arsenal), Shaun Wright-Phillips (Manchester City), Ashley Young (Aston Villa)
Carlton Cole (West Ham United), Peter Crouch (Portsmouth), Jermain Defoe (Tottenham Hotspur), Emile Heskey (Aston Villa), Wayne Rooney (Manchester United)

No comments:

Powered By Blogger