Saturday 30 May 2009

Republic of Ireland 1 Nigeria 1

Timu za Taifa za Republic of Ireland na Nigeria jana zilitoka suluhu ya bao 1-1 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Uwanja wa Klabu ya Fulham, Craven Cottage huko London.
Nigeria ndio walifunga kwanza kupitia Eneramo kwenye dakika ya 30 lakini Ireland wakasawazisha dakika ya 38 mfungaji akiwa Robbie Keane.
Timu zilikuwa: [Kwenye mabano ni Wachezaji wa Akiba walioingizwa na dakika ya mchezo]
Ireland: Shay Given [Keiren Westwood, 46], Kevin Foley [Paul McShane, 72], Richard Dunne, Sean St Ledger, Eddie Nolan, Damien Duff [Aiden McGeady, 46], Liam Miller, Keith Andrews [Glenn whela, 59], Liam Lawrence [Stephen Hunt, 81], Robbie Keane [Shane Long, 46], Leon Best.
Nigeria: Austin Ajide, Olubayo Adefemi, Sam Sodje [Obinna nWaneri, 78], Yusuf Mohamed, Seyi Olofinjana, Sone Alouko [Nsofor Victor Obinna, 60], Kalu Uche, Dele Adeteye, John Utaka, Joseph Akpala [Peter Osaze Odemwingie, 60], Mike Eneramo.
Scholes adokeza huenda akaenda Stoke City kuwa Kocha-Mchezaji!!!
Veterani na Kiungo maarufu wa Manchester United, Paul Scholes, miaka 34, amedokeza kuwa huenda akaenda Klabu ya Stoke City mkataba wake na Manchester United utakapoisha mwakani.
Scholes alianza kuchezea Manchestet United tangu akiwa mdogo.
Scholes anategemewa kumalizia masomo yake ya Ukocha majira ya sasa ya joto wakati msimu wa ligi umemalizika.
Scholes alianza kuchukua mafunzo ya Ukocha, kama ilivyo desturi ya Wachezaji wengi wakongwe wa Man U kama vile Ole Gunnar Solskjaer, Giggs na Neville, misimu kadhaa ya nyuma.
LEO FAINALI YA KOMBE LA UJERUMANI: Werder Bremen v Bayer 04 Leverkusen!!!

Ndani ya Uwanja uitwao Olympiastadion huko Munich, leo Werder Bremen na Bayer 04 Leverkusen zinapambana kwenye Fainali ya kugombea Kombe la Ujerumani linaloshindaniwa na Klabu za Ujerumani.
Werder Bremen ambao wiki moja iliyopita walibwagwa 2-1 kwenye Fainali ya UEFA CUP na Timu ya Ukraine Shakhtar Donetsk watataka kushinda Kombe hili ili kupata nafasi ya kucheza kwenye mashindano mapya ya Ulaya yatayoanza msimu ujao ambayo ndiyo yatachukua nafasi ya UEFA CUP.
Mashindano hayo yatajulikana kama UEFA EUROPA LEAGUE.
Kwa Bayer 04 Leverkusen hali ni kama ya Werder Bremen kwani wao walimaliza Bundesliga wakiwa nafasi ya 9 huku Werder Bremen nafasi ya 10 na nafasi pekee ya kuweza kucheza Ulaya ni kushinda Kombe hili la Ujerumani.
Kwa Wachezaji wawili wa Werder Bremen, Frank Baumann na Diego [pichani] hii ni nafasi yao ya mwisho kwani Baumann anastaafu na Diego, ambae ni Mbrazil, amenunuliwa na Juventus ya Italia.

No comments:

Powered By Blogger