Saturday 30 May 2009

SCOTLAND: Baada ya Ubingwa, leo Rangers wabeba Kombe la Scotland!!
Rangers leo wamelibeba Kombe la Scotland walipowafunga Falkirk katika Fainali iliyochezwa Hampden Park na hivyo kufanikiwa kuchukua Vikombe viwili msimu huu baada ya wiki iliyopita kushinda Ubingwa wa Scotland uliokuwa ukishikiliwa na Mahasimu wao wakubwa Celtic.
Bao la ushindi la Rangers lilipachikwa na Mchezaji Nacho Novo alieingia kama Mchezaji wa Akiba na dakika moja tu baada ya kipindi cha pili kuanza akafunga goli hilo kwa shuti la juu la mbali sana.

No comments:

Powered By Blogger