Monday 25 May 2009

REFA ALIECHEZESHA NUSU FAINALI YA MWAKA JANA HUKO NOU CAMP YA BARCELONA V MAN U KUCHEZESHA FAINALI JUMATANO!!!!

UEFA imemtangaza Refa kutoka Switzerland, Massimo Busacca [pichani], kuwa ndio Mwamuzi wa Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE huko Roma, Italia siku ya Jumatano kati ya Mabingwa Watetezi wa Kombe hilo Manchester United na Barcelona itakayochezwa ndani ya Stadio Olimpico. Busacca, miaka 40, atasaidiwa na Matthias Arnet na Francesco Buragina pia kutoka Switzerland na Mwamuzi wa nne ambae ni wa Akiba ni Claudio Circhetta nae pia kutoka Switzerland.
Wadau wanaweza kumkumbuka Refa huyu ndie aliechezesha pambano la mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu uliopita huko Nou Camp kati ya Barcelona na Manchester United, mechi iliyoisha 0-0, na katika mechi hiyo aliwapa penalti Manchester United kipindi cha kwanza lakini Ronaldo alikosa.
Lakini baadae, kipindi hicho hicho cha kwanza, aliwanyima Manchester United penalti ya wazi kabisa baada ya Ronaldo kuangushwa ndani ya boksi na baada ya mechi Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson alisema: 'Dunia nzima pamoja na Mkewe wanajua ile ni penalti!! Lakini kwenye mechi kama hizi ukipata penalti moja ni majaliwa, mbili ni maajabu makubwa!!!'
Hata hivyo, Busacca ameshachezesha mechi ya Manchester United msimu huu na ni ile mechi ya marudiano ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kule Porto ambayo Man U waliwabwaga nje FC Porto kwa kuwafunga 1-0 nyumbani kwake.

No comments:

Powered By Blogger