Friday 29 May 2009

Mkataba wa Torres waboreshwa!!!
Mkataba wa Fernando Torres umeboreshwa na Klabu yake ya Liverpool na vilevile kuongezewa kipengele cha kuurefusha hadi msimu wa mwaka 2013/14.
Mshambuliaji huyu kutoka Spain alichukuliwa na Liverpool toka Atletico Madrid na mpaka sasa ameifungia Liverpool mabao 50.
Mpaka sasa Dirk Kuyt, Daniel Agger, Steven Gerrard na Meneja Rafa Benitez wamesaini mikataba mipya.
Dwight Yorke kumwagwa na Sunderland!!
Mkongwe Dwight Yorke ni miongoni mwa Wachezaji 7 ambao wataachwa na Klabu ya Sunderland ambayo inataka kujijenga upya baada ya kunusurika kushushwa Daraja.
Wengine ni david Connolly, Arnau Riera, Darren Ward, Nick Colgan, Peter Hartley na Niall McArdle.
Steven Ireland asaini mkataba mpya Man City
Kiungo wa Manchester City, Steven Ireland, amesaini mkataba mpya wa miaka mitano utakaomweka hapo hadi mwaka 2014.
Ireland ndie Mchezaji aling'ara sana Man City msimu huu.

No comments:

Powered By Blogger