Saturday 30 May 2009

Juninho aondoka Lyon kwa machozi!!

Kiungo wa zamani wa Brazil, Juninho Pernambucano, ataondoka Klabu ya Lyon baada ya msimu huu kumalizika leo baada ya kukaa Klabu hiyo ya Ufaransa tangu 2001 na kuwasaidia kuchukua Ubingwa mara 7.
Mwenyekiti wa Lyon, Jean-Michel Aulas, amesema ingawa mkataba wa Juninho, mwenye umri wa miaka 34, utaisha msimu ujao lakini kwa yale yote aliyoifanyia Lyon wameamua kumruhusu aondoke mapema kama ‘mtu huru’.
Aulas alitamka: ‘Juninho anaondoka!’
Kauli hiyo ya Mwenyekiti ilimfanya Juninho alieketi pembeni yake kububujikwa machozi.
Juninho aliifungia Lyon goli lake la 100 Jumamosi iliyopita walipoifunga Caen 3-1.
Juninho aliichezea Brazil mechi 44 na kufunga goli 7.

No comments:

Powered By Blogger