Saturday 17 October 2009

Aston Villa 2 Chelsea 1
Wakiwa uwanjani kwao Villa Park, Aston Villa wamewafunga vinara wa Ligi Kuu England, Chelsea, mabao 2-1 katika mechi ya leo iliyoanza mapema.
Hadi mapumziko mabao yalikuwa 1-1.
Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kufunga kwa mkwaju wa mbali wa Didier Drogba uliodunda mbele ya Kipa Brad Friedel na kutinga wavuni.
Richard Dunne aliisawazishia Aston Villa kwa kichwa baada ya kona na kipindi cha pili ni kona nyingine tena iliyowapa Aston Villa ushindi kupitia Mlinzi James Collins aliefunga kwa kichwa.
VIKOSI vilikuwa:
Aston Villa: Friedel, Cuellar, Collins, Dunne, Warnock, Petrov, Milner, Sidwell, Ashley Young, Carew, Agbonlahor. AKIBA: Guzan, Delph, Heskey, Reo-Coker, Shorey, Beye, Gardner.
Chelsea: Cech, Bosingwa, Carvalho, Terry, Ashley Cole, Essien, Malouda, Lampard, Deco, Anelka, Drogba. AKIBA: Hilario, Ivanovic, Joe Cole, Zhirkov, Kalou, Sturridge, Belletti.

No comments:

Powered By Blogger