Saturday 17 October 2009

GOLI LA PUTO JEKUNDU LAIUA LIVERPOOL!!!
Goli la dakika ya 5 Mfungaji akiwa Darren Bent aliepiga shuti na kugonga puto lililorushwa uwanjani na Shabiki wa Liverpool na kumbabaisha Kipa wa Liverpool Pepe Reina huku mpira ukipita kushoto kwake na puto kupita kulia limewapa ushindi Sunderland wakiwa nyumbani Stadium of Light.
Puto hilo lilimbabaisha Kipa Reina ambae alionekana kutaka kudaka puto badala ya mpira na Wachezaji wa Liverpool walilalamika lakin Refa aliamua ni goli halali.
Liverpool, wakicheza bila ya mihimili yao Nahodha Steven Gerrard na Straika Fernando Torres, kipigo cha leo ni cha nne kwa msimu huu.
Mabingwa MAN U washinda 2-1 na kutinga kileleni!!!
Ndani ya Old Trafford, Manchester United, leo wameifunga Bolton Wanderers 2-1 na kuchukua uongozi wa Ligi Kuu wakiwa na pointi 22 na kufuatiwa na Chelsea, waliofungwa na Aston Villa 2-1 leo, wakiwa na pointi 21.
Goli la kwanza lilifungwa dakika ya 5 baada ya kichwa cha Michael Owen kumbabatiza Beki Zat Knight na bao la pili alifunga Antonio Valencia dakika ya 33 likiwa ni goli lake la kwanza kwa Winga huyo kuifungia Man U.
Bao la Bolton lilifungwa na Matty Taylor kwa kichwa dakika ya 75.
Vikosi vilikuwa:
Man Utd: Van der Sar, Neville, Ferdinand, Jonathan Evans, Evra, Valencia, Carrick, Anderson, Giggs, Owen, Berbatov. AKIBA: Kuszczak, Brown, Nani, Scholes, Welbeck, O'Shea, Macheda.
Bolton: Jaaskelainen, Ricketts, Knight, Cahill, Samuel, Lee, Cohen, Muamba, Gardner, Taylor, Kevin Davies.
AKIBA: Al Habsi, Robinson, Steinsson, Mark Davies, Klasnic, McCann, Basham.
Refa: Mark Clattenburg
Arsenal 3 Birmingham 1
Wakiwa kwao Emirates Stadium Arsenal wameifunga Birmingham 3-1 na sasa wako nafasi ya 4 wakiwa na pointi 18 kwa mechi 8.
Magoli ya Arsenal yaligungwa na Van Persie dakika ya 16, diaby ya 18 na Arshavin dakika ya 84.
Bao la Birmingham lilifungwa na Lee Bowyer dakika ya 38.
RATIBA LIGI KUU:
Jumapili, Oktoba 18: [saa za bongo]
Blackburn v Burnley [saa 9 mchana]
Wigan v Man City [saa 12 jioni]
Jumatatu, Oktoba 19
Fulham v Hull City

No comments:

Powered By Blogger