Sunday 18 October 2009

Fergie aongea kuhusu Refa Alan Wiley
Sir Alex Ferguson ametoboa kuwa alimponda Refa Alan Wiley na kumwita hayuko fiti baada ya mechi ya Ligi Kuu ya Timu yake Manchester United na Sunderland kumalizika 2-2 kwa sababu alikerwa na uchezaji wa Timu yake uliokuwa chini ya kiwango na walibahatika kupata suluhu baada ya goli la kujifunga mwenyewe kwa Beki wa Sunderland Anton Ferdinand, ambae ni mdogo wake mlinzi wa Man U Rio Ferdinand, dakika za majeruhi.
Sir Alex Ferguson ameshaomba radhi kwa kauli yake hiyo na pia ameshajieleza kimaandishi kwa FA, kama alivyoamriwa, na sasa Jumatatu Oktoba 19 atajua kama FA itamfungulia mashitaka au la.
Ferguson amesema: “Niliudhika na uchezaji wetu mbovu na hasira zilinifanya nimlaumu Refa Wiley! Ndio maana nikaona ni bora niombe radhi kwake! Nadhani atakubali kuomba kwangu msamaha na na ntajaribu kuongea nae uso kwa uso!”
GOLI LA PUTO JEKUNDU LISINGEKUBALIWA!
Refa wa zamani wa Ligi Kuu, Jeff Winter, ameshangazwa kwa kukubaliwa goli la Sunderland hapo jana walipoifunga Liverpool bao 1-0 kwani mpira uliopigwa kwenye dakika ya 5 ya mchezo na Straika Darren Bent wa Sunderland uligonga ‘mpira mwekundu wa bichi’ na kumbabaisha Kipa Pepe Reina wa Liverpool na kutinga wavuni. Mpira huo wa ‘bichi’ ulitupwa na Shabiki mmoja wa Liverpool aliekaa nyuma ya goli sekunde chache kabla tukio la goli.
Jeff Winter amesema: “Sheria za Soka ziko wazi! Kama kunatokea kitu nje ya uwanja na kuingilia mchezo basi ni wajibu wa Refa kusimamisha mchezo hadi kitu hicho kinaondolewa! Nadhani Marefa wa mechi hiyo walijua hilo lakini wamekosea kwa kulikubali goli!”
Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, amekataa kulaumu ‘mpira huo wa bichi’ kwa kufungwa na alikri kuwa Timu yake haikucheza vizuri.
Jana Liverpool iliwakosa nguzo yao, Nahodha Steven Gerrard na Straika Fernando Torres, ambao ni majeruhi.

No comments:

Powered By Blogger