Sunday 18 October 2009


HILI NDIO GOLI LA 'PUTO JEKUNDU!!!'
Pichani Kipa Pepe Reina wa Liverpool akibabaika adake mpira au 'puto jekundu' kwenye mechi ya jana ya Ligi Kuu ambayo Liverpool ikiwa ugenini ilifungwa na Sunderland bao 1-0 kwa goli ambalo sasa limebatizwa "GOLI LA PUTO JEKUNDU!".
'Puto' hilo, hakika ni mpira wa kuchezea bichi, ulitupwa uwanjani na Shabiki mmoja wa Liverpool alieketi nyuma ya goli na sekunde chache baadae Darren Bent wa Sunderland kupiga shuti lililoubabatiza mpira huo wa bichi na kumwacha Reina akitaka kudaka 'puto' hilo na mpira kutinga wavuni.

No comments:

Powered By Blogger