Thursday 22 October 2009

Chelsea waomba kifungo kisimamishwe hadi rufaa yao iishe!!
Chelsea wameiomba CAS [Court of Arbitration for Sport], Mahakama ya Usuluhishi Michezoni, isimamishe adhabu waliyopewa na FIFA ya kutosajili Wachezaji hadi 2011 kwa kosa la kumrubuni na kumsajili kinyume cha sheria Chipukizi kutoka FC Lens ya Ufaransa, Gael Kakuta, mwaka 2007 hadi hapo uamuzi wa rufaa yao kwa CAS utakapotolewa.
Kakuta, ambae sasa ana miaka 18, amefungiwa miezi minne na kutakiwa kuilipa fidia FC Lens Pauni 710,000.
Chelsea imetakiwa pia iilipe FC Lens Pauni 118000 kama fidia ya kumfundisha Kakuta.
CAS bado haijapanga lini itasikiliza rufaa hiyo ya Chelsea.
Wachezaji wa Ujerumani kuvaa Vesti za Deraya ili kuzuia risasi huko Bondeni!!
Wachezaji wa Ujerumani watakaokuwa Kikosi cha Ujerumani cha Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwakani kwenye Fainali wameambiwa iwatalazimu kuvaa vesti za kuzuia risasi ikiwa watataka kutoka nje ya Hoteli watakayofikia huko Afrika Kusini.
Mkuu wa Ulinzi wa Kampuni ya BaySecur ambayo huwalinda Chama cha Soka cha Ujerumani na wageni zake amesema inabidi Wachezaji wawe waangalifu zaidi Afrika Kusini hasa kwa vile ujambazi umekithiri na ikiwalazimu kutoka nje ya Hoteli yao basi inabidi wapewe eskoti yenye silaha na Wachezaji wavae vesti hizo za kuzuia risasi.
Chakula cha Man U chaharibiwa na Idara ya Forodha Urusi!!!!
Chakula cha kwenye ndege ambayo ilikwenda kuwabeba Manchester United huko Moscow, Urusi ili kuwarudisha Manchester mara baada ya kuwafunga CSKA Moscow 1-0 katika mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE hapo jana kiliamriwa kiharibiwa na Idara ya Forodha ya Uwanja wa Moscow kwani uingizwaji wake ulikiuka kanuni za Urusi.
Chakula hicho maalum kiliagizwa na Uongozi wa Manchester United na kilikuwa na lishe maalum ili kuwawezesha Wachezaji kujenga miili yao baada ya mechi yao na CSKA hasa ukichukulia wana mechi ya Lig Kuu na Mahasimu wao wakuu Liverpool siku ya Jumapili huko Anfield.
Wachezaji wa Manchester United walitegemewa kupata mlo huo wakiwa kwenye safari kutoka Moscow kurudi Manchester ambayo huchukua masaa manne.
Parreira: Afrika Kusini wakinipa ofa ntaifikiria!
Carlos Alberto Parreira amesema akipewa ofa na Afrika Kusini ili kuwa Kocha wa Bafana Bafana ataifikiria ipasavywo.
Afrika Kusini ndio Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa kuanzia Juni 11, 20010 hadi Julai 11, 2010 na kwa sasa hawana Kocha baada ya kumtimua Mbrazil mwenzake Parreira, Joel Santana ambae alishika wadhifa huo kutoka kwa Parreira alielazimika kuuacha baada ya Mke wake kuugua mwaka jana.
Hata hivyo, kipindi cha Santana, Bafana Bafana ilifungwa mechi 8 kati ya 9 ilizocheza mwisho na hilo ndilo lilimfanya atimuliwe.
Parreira, aliyekuwa Kocha wa Brazil iliyochukua Kombe la Dunia mwaka 1994, amesema: “Kuna chansi ntapewa ofa! Ntaiangalia! Wao wanataka waendelee na Kocha wa Brazil kwani wanaamini staili ya Brazil ndio inayoifaa Afrika Kusini. Kocha atakaeichukua Afrika Kusini atalazimika kuondoa balaa la kufungwa! Morali ni ndogo kwao!”

No comments:

Powered By Blogger