Wednesday 21 October 2009

TATHMINI-UEFA CHAMPIONS LEAGUE LEO:
RATIBA: Jumatano, Oktoba 21
Bordeaux v Bayern Munich,
CSKA Moscow v Manchester United
Chelsea v Atletico Madrid,
FC Porto v Apoel Nicosia,
FC Zurich v Marseille,
Juventus v Maccabi Haifa,
Real Madrid v AC Milan,
Wolfsburg v Besiktas,
Manchester United wako ugenini Urusi kucheza na CSKA Moscow kwenye Uwanja wa Luzhniki wenye nyasi bandia ambao huwa mgumu kuchezea kwa timu ngeni.
Mechi hii itaanza mapema kupita zote na itaanza saa 1 na nusu usiku saa za bongo.
Hata hivyo, Manchester United wanaukumbuka vyema uwanja huo kwani Mei 2008 ndipo waliponyakua Kombe la UEFA CHAMPIONS LEAGUE walipowabwaga Chelsea.
Man U wako huko Moscow bila Mastaa wao Giggs, Rooney, Evra, Fletcher na Park ambao wameachwa Manchester kwa kuwa ni majeruhi.
Mpaka sasa kwenye Kundi lao Man U ndio wako juu baada ya kuzishinda Besiktas na Wolfsburg katika mechi mbili za kwanza.
CSKA Moscow, wanafundishwa na Kocha wa zamani wa Tottenham Juande Ramos, wameshinda mechi moja na kufungwa moja. Walifungwa na Wolfsburg na wao kuifunga Besiktas.
Katika Kundi hili B mechi nyingine ya leo ni kati ya Wolfsburg na Besiktas.
Kundi D, Chelsea wanaoongoza Kundi hili wapo nyumbani Stamford Bridge na watacheza na Atletico Madrid.
Katika mechi nyingine ya Kundi hilI FC Porto watawakaribisha Apoel Nicosia huko Ureno.
Kundi C, leo ni mechi ya Miamba Real Madrid na AC Milan mechi inayochezwa nyumbani kwa Real Uwanjani Santiago Bernabeu.
Katika mechi hiyo, Nyota wa Brazil Kaka leo, kwa mara ya kwanza, atapambana na Klabu yake ya zamani AC Milan.
Mechi nyingine ya Kundi C ni kati ya FC Zurich na Marseille.
Real Madrid ndie anaeongoza Kundi C huku FC Zurich akifuatia.
Mechi za Kundi A za leo ni Bordeaux v Bayern Munich na juventus v Maccabi Haifa.
Bayern Munich ndie anaongoza Kundi hili akiwa pointi sawa na Bordeaux lakini bAyern yuko mbele kwa magoli.
JANA-USIKU WA MAAJABU ULAYA!!!
MASKINI: Liverpool ni vipigo mfululizo!!!! Barca waaibishwa Nou Camp!!!
Mechi za jana za UEFA CHAMPIONS LEAGUE zimeleta matokeo yasiyotarajiwa na magoli bwelele huku ajabu kubwa ni pale Warusi Rubin Kazan walipowakung’uta Mabingwa Watetezi wa Ulaya FC Barcelona kwa bao 2-1 tena wakiwa nyumbani kwao Nou Camp.
Liverpool wameendelea kupata vipigo mfululizo ingawa jana sio puto ndio liliwafunga bali ni goli la dakika za majeruhi wakiwa kwenye ngome yao Anfield na pia kupata athari kubwa pale mhimili wao na Nahodha wao Steven Gerrard kucheza dakika 25 tu za mwanzo na kulazimika kutoka baada ya kuumia.
Matokeo ya mechi ya jana ambayo Liverpool alifungwa 2-1 na Lyon ya Ufaransa yamedhihirisha ile imani ya wengi kuwa Liverpool bila Gerrard na Torres ni nyanya tu. Jana Torres hakucheza kabisa.
Sasa, baada ya vipigo mfululizo, Jumapili kwenye Ligi Kuuu, Liverpool wanawakaribisha Mahasimu wao wakubwa Manchester United na hilo linawatia homa Mashabiki wa Liverpool.
Arsenal wakiwa ugenini huko Uholanzi na huku wakiongoza bao 1-0 walilazimishwa sare ya 1-1 na AZ Alkmaar.
Rangers ya Scotland iliadhiriwa vibaya ikiwa nyumbani baada ya kuchapwa bao 4-1 na Unirea Urziceni.
Sevilla, baada ya mechi 3 tu, wameweka rekodi huko Ulaya baada ya kufuzu kusonga mbele Raundi nyingine baada ya mechi 3 tu.
Matokeo kamili mechi za jana Jumanne, Oktoba 20:
KUNDI E
Liverpool 1 Lyon 2
Debrecen 3 Fiorentina 4
KUNDI F
Inter Milan 2 Dynamo Kiev 2
Barcelona 1 Rubin Kazan 2
KUNDI G
Stuttgart 1 Sevilla 3
Rangers 1 Unirea Urziceni 4
KUNDI H
AZ Alkmaar 1 Arsenal 1
Olympiakos 2 Standard Liege 1

No comments:

Powered By Blogger