Wednesday 21 October 2009

Misri kupasha na Bongo!!!
Timu ya Taifa ya Misri imejitoa kucheza na Ujerumani mechi ya kirafiki mwezi ujao na badala yake itacheza na Tanzania kabla ya pambano lao la kufa na kupona na Algeria la Kombe la Dunia la kuwania nani ataenda Fainali Kombe la Dunia.
Mechi hiyo kirafiki kati ya Misri na Tanzania itachezwa Novemba 5 na taarifa za mechi zimethibitishwa na Kocha Msaidizi wa Misri Shawki Gharib aliesema: “Tumeamua kucheza na Tanzania ingawa mechi hiyo haipo kwenye Kalenda ya FIFA ya mechi za Kimataifa. Hio ndio sababu kwa vile Tanzania haina Wachezaji wanaocheza nje na inakuwa rahisi kucheza nao nje ya Kalenda ya FIFA.”
Algeria wako pointi 3 mbele ya Misri kwenye Kundi lao na mechi hiyo kati ya Misri na Algeria itakayochezwa Cairo ni muhimu kwa Misri wanaohitahi ushindi wa 3-0 ili kwenda Fainali Kombe la Dunia.
Katika mechi ya mwisho ya Kundi lao, Misri waliifunga Zambia 1-0 huko Lusaka.

No comments:

Powered By Blogger