Monday 19 October 2009

Refa aliekubali “GOLI LA PUTO” abwagwa kuchezesha Daraja la chini Wikiendi ijayo!!
Refa Mick Jones aliechezesha mechi ya Ligi Kuu kati ya Sunderland na Liverpool Jumamosi iliyopita na kukubali goli lililofungwa baada ya mpira kuugonga ‘mpira wa bichi’ uliotupwa uwanjani na Shabiki wa Liverpool na kumbabaisha Kipa Pepe Reina, ameondolewa kuchezesha Ligi Kuu na badala yake atachezesha mechi ya Daraja la Chini kati ya Peterborough na Scurnthorpe.
Ingawa Kipa Pepe Reina na wenzake walilalamika Refa huyo alilikubali goli hilo kinyume na sheria.
Fergie ashitakiwa na FA!!!
Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, ametakiwa ajibu mashitaka ya “kutokuwa na mwenendo wa kuridhisha” ifikapo Novemba 3 kufuatia kauli aliyoitoa hapo Oktoba 3 mara baada ya mechi ya Man U na Sunderland iliyoisha 2-2 pale alipomsema Refa Alan Wiley hayuko fiti kuchezesha mechi kwa kuwa alikuwa akichukua muda mwingi kuwaonya, kuwapa Kadi na kuwaandika Wachezaji kwenye kitabu muda ambao ulimsaidia kupumzika.
Licha ya Sir Alex Ferguson kuomba radhi kwa kauli yake na pia kuiandikia FA kujieleza, leo FA imetangaza lazima ajibu mashitaka.
Endapo Ferguson atapatikana na hatia basi anaweza kupigwa faini au kuufungiwa kukaa kwenye benchi la ufundi wakati wa mechi au vyote viwili kwa pamoja.
Droo ya Mitoano ya Nchi za Ulaya kuwania nafasi 4 kutinga Fainali Kombe la Dunia 2010 yafanyika!!!
Mechi za Mtoano wa Nchi 8 za Ulaya zimepangwa leo ili kupata Timu 4 zitakazoenda Fainali Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na mechi hizo zitachezwa nyumbani na ugenini hapo Novemba 14 na marudio ni Novemba 18.
RATIBA:
Novemba 14
Republic of Ireland v France
Portugal v Bosnia-Hercegovina
Greece v Ukraine
Russia v Slovenia
Novemba 18
France v Republic of Ireland
Bosnia-Hercegovina v Portugal
Ukraine v Greece
Slovenia v Russia
Man U waenda Moscow leo bila Wachezaji Watano muhimu!!!
Rooney, Giggs waachwa!!!
Kikosi cha Manchester United leo kilipanda ndege kuelekea Moscow, Urusi ambako Jumatano watacheza na CSKA Moscow kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE bila ya Wachezaji wao watano maarufu wakiwemo Ryan Giggs na Wayne Rooney ambao ni majeruhi.
Wachezaji wengine walioachwa ni Patrice Evra, Park Ji-Sung na Darren Fletcher ambao pia ni majeruhi.
Ingawa Dimitar Berbatov na Nemanja Vidic walikuwamo kwenye msafara lakini hawana uhakika kama watachezeshwa kwa vile nao pia ni majeruhi.
Kikosi kilichopanda ndege ni:
Van der Sar, Kuszczak, Foster; Neville, Rafael, O'Shea, Ferdinand, Vidic, Brown, J Evans, Fabio; Valencia, Scholes, Carrick, C Evans, Anderson, Nani; Owen, Berbatov, Macheda, Welbeck.

No comments:

Powered By Blogger