Sunday 18 October 2009

Wigan 1 Man City 1
Mechi ya Ligi Kuu kati ya Wigan na Manchester City ndani ya KC Stadium, nyumbani kwa Wigan iliyochezeshwa na Refa Alan Wiley ambae wiki mbili sasa yuko kwenye vichwa vya habari Magazetini baada ya mzozo unaomhusu Sir Alex Ferguson, ilimalizika kwa sare ya 1-1 na Man City kuwa mtu 10 baada ya Refa Alan Wiley kumpa Kadi 2 za Njano Mlinzi toka Argentina Pablo Zabaleta.
Wigan walitangulia kufunga bao la kwanza dakika ya 45 mfungaji akiwa Charles N'Zogbia lakini Man City walirudisha dakika moja tu baada ya kipindi cha pili kuanza kupitia Martin Petrov.
VIKOSI:
Wigan: Kirkland, Melchiot, Boyce, Bramble, Figueroa, Rodallega, Thomas, Diame, N'Zogbia, Scharner, Scotland.
AKIBA: Pollitt, Cho, Koumas, Gomez, Sinclair, Kapo, King.
Man City: Given, Zabaleta, Richards, Lescott, Bridge, Wright-Phillips, De Jong, Barry, Petrov, Tevez, Adebayor. AKIBA: Taylor, Johnson, Ireland, Santa Cruz, Sylvinho, Kompany, Weiss.
Refa: Alan Wiley

No comments:

Powered By Blogger