Thursday 22 October 2009

LEO EUROPA LIGI!!
Baada ya kunguruma kwa UEFA CHAMPIONS LIGI jana na juzi, leo ni zamu ya EUROPA LIGI kutawala anga za Ulaya kwa mechi kadha wa kadha.
Timu za Uingereza zitazoshuka dimbani leo ni Everton, Fulham na Celtic.
Mechi zao ni:
Benfica v Everton
Fulham v AS Roma
Celtic v Hamburger SV
MECHI NYINGINE NI:
Ajax v Dinamo Zagreb,
Athletic Bilbao v Nacional,
BATE v AEK Athens,
Club Brugge v Partizan Belgrade,
CSKA Sofia v Basle,
FC Sheriff Tiraspol v FC Twente,
FK Austria Vienna v Werder Bremen,
FK Ventspils v Sporting,
Galatasaray v Dinamo Bucharest,
Hapoel Tel-Aviv v Rapid Vienna,
Hertha Berlin v Heerenveen,
Lazio v Villarreal,
Lille v Genoa,
Panathinaikos v SK Sturm Graz,
Politehnica Timisoara v Anderlecht,
PSV v FC Copenhagen,
Shakhtar Donetsk v Toulouse,
Sparta Prague v CFR 1907 Cluj-Napoca,
Steaua Bucharest v Fenerbahce,
SV Red Bull Salzburg v Levski Sofia,
Valencia v Slavia Prague,
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Mechi za Jana!!!
Real Madrid wabamizwa kwao, Chelsea ushindi mnono na Bayern apigwa!!
KUNDI C
Makosa ya Makipa wa pande zote mbili, jana walifanya mechi ya Real Madrid na AC Milan iwe na lundo la magoli lakini alikuwa Chipukizi toka Brazil, Pato, alieipa ushindi AC Milan wakiwa ugenini Uwanjani Santiago Bernabeu.
Mechi hii iliisha kwa ushindi wa AC Milan wa bao 3-2.
Katika mechi nyingine ya Kundi hili, Mchezaji wa zamani wa Real Madrid na Manchester United, Mlinzi Gabriel Heinze aliipa ushindi Klabu yake Marseille wa bao 1-0.
KUNDI A
Bordeaux waliifunga Bayern Munich 2-1 katika mechi iliyokuwa na goli la kujifunga, penalti 2 kukoswa na Kadi Nyekundu 2.
Bayern waliongoza kwenye dakika ya 6 baada ya Michael Ciani kujifunga mwenyewe lakini Ciani alijirekebisha na kuisawazishia Bordeaux.
Bayern wakabaki mtu 10 baada ya Thomas Mueller kupewa Kadi 2 za Njano na hivyo kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu na dakika 5 kabla mapumziko, Marcus Planus akaifungia Bordeaux bao la pili.
Kisha Yoann Gourcuff akakosa penalti ya kwanza ya Bordeaux na akafuata Daniel van Bueyten wa Bayern kupewa Kadi Nyekundu baada ya kumchezea faulo Marouane Chamakh ndani ya boksi lakini penalti iliyopigwa na Jussie haikuzaa goli kwa Bordeaux na hivyo kukosa penalti 2 katika mechi hiyo.
Katika mechi nyingine ya Kundi hili Juventus waliifunga Maccabi Haifa 1-0.
KUNDI D
Chelsea wakiwa nyumbani Stamford Bridge waliishindlia Atletico Madrid mabao 4-0 kwa mabao ya Salomon Kalou, mawili, Frank Lampard na la kujifunga mwenyewe la Luis Perea.
FC Porto waliifunga Apoel Nicosia 2-1.
KUNDI B
Wolfsburg walitoka suluhu 0-0 na Besiktas na Manchester United walishinda ugenini 1-0 dhidi ya CSKA Moscow.

No comments:

Powered By Blogger