Sunday 18 October 2009

Blackburn 3 Burnley 2
Katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu England kati ya mbili za leo Jumapili Oktoba 18, Blackburn Rovers wakiwa nyumbani Ewood Park, wamejinyakulia pointi 3 baada ya kuwapiga Burnley bao 3-2.
Burnley ndio walikuwa wa kwanza kufunga bao kwenye dakika ya 5 kupitia Robbie Black lakini Blackburn wakasawazisha dakika 3 baadae mfungaji akiwa Richard Dunne.
Dakika ya 20 Blackburn wakaongeza bao la pili mfungaji akiwa Straika wa Ureno Di Santo na Pascal Chimbonda akaipatia bao la 3 dakika ya 40.
Burnley walipata bao la pili kwenye dakika ya 90 mfungaji akiwa Mchezaji wa zamani wa Man U Chris Eagles na kuifanya mechi iwe patashika katika dakika za majeruhi huku Burnley wakipigana kusawazisha.
Mechi ya pili itakayoanza muda si mrefu kuanzia sasa ni kati ya Wigan na Manchester City.

No comments:

Powered By Blogger