Tuesday 20 October 2009

Fergie kwenda kujitetea mwenyewe kesi yake FA!!!
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ataomba kwenda kutoa utetezi wake mwenyewe wakati kesi yake aliyoshitakiwa na FA itakaposikilizwa.
Ferguson ameshitakiwa kwa kosa la ‘kuonyesha mwenendo usioridhisha’ baada ya kutoa matamshi tarehe 3 Oktoba kwamba Refa Alan Wiley aliechezesha mechi ya Ligi Kuu kati ya Manchester United na Sunderland iliyoisha 2-2 hakuwa fiti.
Ingawa Ferguson aliomba radhi kwa kauli yake kwa Refa Alan Wiley, FA iliamua kumshitaki na amepewa mpaka Novemba 3 kuwasilisha utetezi wake.
Wiki iliyopita FA ilimpa onyo badala ya faini au kifungo au vyote Meneja wa Liverpool Rafa Benitez kwa shitaka kama la Ferguson kwa vile ana rekodi nzuri lakini Wadadisi wa mambo wanahisi Sir Alex Ferguson itakuwa ngumu kwake kukwepa adhabu kali hasa kwa vile siku za nyuma ameshawahi kupatikana na hatia kwa kosa kama hilo pale alipopigwa Faini Pauni 5000 baada ya kumvaa Refa Mark Clattenburg haftaimu kwenye mechi na Bolton misimu miwili iliyopita.
Pia ashawahi kufungiwa mechi mbili baada ya kukwaruzana na Refa Mike Dean kwenye mechi ambayo Man U waliifunga Hull City.

No comments:

Powered By Blogger