Tuesday 20 October 2009

UEFA CHAMPIONS LEAGUE kunguruma leo Ulaya!!:
Leo ni Liverpool v Lyon na AZ Alkmaar v Arsenal
Jumanne, 20 Oktoba 2009
[saa 3 dak 45 usiku]
AZ Alkmaar v Arsenal,
Barcelona v Rubin Kazan,
Debrecen v Fiorentina,
Inter Milan v Dynamo Kiev,
Liverpool v Lyon,
Olympiakos v Standard Liege,
Rangers v Unirea Urziceni,
VfB Stuttgart v Sevilla,
KESHO:
Jumatano, 21 Oktoba 2009
Bordeaux v Bayern Munich,
CSKA Moscow v Manchester United
Chelsea v Atletico Madrid,
FC Porto v Apoel Nicosia,
FC Zurich v Marseille,
Juventus v Maccabi Haifa,
Real Madrid v AC Milan,
Wolfsburg v Besiktas,
Tathmini:
Liverpool v Lyon
Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard yuko fiti kucheza mechi ya leo ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE nyumbani Anfield lakini Straika Fernando Torres ataikosa mechi hii kwa vile bado ni majeruhi.
Wachezaji wote hao wawili hawakucheza Jumamosi kwenye kipigo cha ‘Goli la Puto” katika mechi ya Ligi Kuu waliyofungwa 1-0 na Sunderland.
Liverpool wako nafasi ya 3 kwenye KUNDI E baada ya kushinda mechi moja na kufungwa moja huku Wapinzani wao wa leo kutoka Ufaransa Lyon ndio wanaongoza kwa kushinda mechi zao mbili za kwanza.
Kipigo cha Liverpool cha Jumamosi mikononi mwa Sunderland ni kipigo chao cha 4 katika Ligi msimu huu lakini Meneja Rafa Benitez amesema: “Tukishinda leo na Lyon, Timu itapata moyo na tukishinda Jumapili ijayo na Manchester United nina uhakika hali yetu itakuwa tofauti kabisa!”
Lyon siku ya Jumamosi kwenye ligi ya kwao Ufaransa walipata kipigo chao cha kwanza msimu huu walipofungwa 2-0 na Sochaux huku wakicheza bila Mastaa wao Sidney Govou, Kim Kallstrom, Cleber Anderson, Mathieu Bodmer na Jean-Alain Boumsong ambao wote wanategemewa kucheza leo.
Kikosi cha Liverpool kitatokana na: Reina, Johnson, Carragher, Agger, Skrtel, Insua, Aurelio, Dossena, Benayoun, Riera, Gerrard, Mascherano, Lucas, Babel, Voronin, Kuyt, Ngog, Spearing, Cavalieri, Darby, Plessis.
AZ Alkmaar v Arsenal
Leo Arsenal watacheza bila Wachezaji majeruhi Tomas Rosicky na Theo Walcott watakapokuwa Uwanjani DSB Stadion huko Uholanzi kucheza na AZ Alkmaar kwenye mechi ya Kundi H ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Wachezaji wengine wa Arsenal watakaokosa mechi ya leo kwa kuwa ni majeruhi ni Samir Nasri, Kipa Lukasz Fabianski, Nicklas Bendtner, Eduardo, Denilson na Johan Djourou.
Ingawa Kipa Manuel Almunia amepona ugonjwa aliokuwa ameumwa lakini huenda akakosa namba kwa vile Kipa Chipukizi Vito Mannone ameonyesha umahiri mkubwa katika mechi alizocheza hadi sasa.
Mpaka sasa katika Kundi H, Arsenal hawajafungwa baada ya kuzishinda TImu za Olympiakos na Standard Liege katika mechi za awali na ndio wanaoongoza Kundi hili.
AZ Alkmaar inafundishwa na Staa wa zamani wa Uholanzi Ronald Koeman na ingawa wako mkiani kwenye Kundi H baada ya kutoka sare mechi moja na kufungwa moja ni wagumu mno kufungika kwao kwani katika mechi 34 za Makombe ya Ulaya walizocheza nyumbani wamefungwa mechi moja tu.
Kikosi cha Arsenal kitatokana na: Mannone, Clichy, Gallas, Vermaelen, Sagna, Eboue, Song, Fabregas, Diaby, Arshavin, van Persie, Almunia, Vela, Gibbs, Silvestre, Merida, Wilshere, Ramsey.
Santana si Kocha tena Bondeni!!!
Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia Afrika Kusini na Kocha wao Joel Santana kutoka Brazil wameafikiana kuvunja mkataba kati yao na kwa hivyo Timu ya Taifa ya Afrika Kusini, maarufu kwa jina la Bafana Bafana au ukipenda siku hizi ‘Watoto wa Vuvuzela’, sasa haina Kocha na Wasaidizi Pitso Mosimane na Jairo Leal wataiongoza Timu hiyo kwa muda.
Uamuzi wa Santana kutengana na Afrika Kusini umetangazwa jana na hilo limefuatia matokeo mabaya ya Bafana Bafana tangu Santana aanze kuifundisha Aprili, 2008 alipochukua nafasi ya Mbrazil mwenzake Carlos Alberto Parreira ambae alilazimika kuondoka kurudi kwao Brazil baada ya kuuguliwa na mkewe.
Rais wa SAFA, Chama cha Soka Afrika Kusini, Kirsten Nematandani, amesema sasa wanatafuta Kocha mwingine haraka iwezekanavyo ili wajiandae vyema kama Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa kuanzia Juni 11 hadi Julai 11 mwakani.

No comments:

Powered By Blogger