Tuesday 20 October 2009

Blatter kuwania tena Urais FIFA 2011!!!
Rais wa FIFA, Sepp Blatter, ametoboa kuwa atasimama tena kwenye uchaguzi wa kugombea Urais FIFA hapo mwaka 2011.
Blatter ambae yupo kwenye wadhifa huo tangu 1998 amesema: “Bado sijakamilisha misheni yangu kwenye Soka!”
Blatter, mwenye umri wa miaka 78 na ni raia wa Uswisi, alichukua wadhifa huo toka kwa Joao Havelange wa Brazil.
Akisisitiza, Blatter ametamka: “Sijamaliza misheni yangu kwenye Soka! Nahitaji muda zaidi! Natumai mwaka 2011, Kongresi ya FIFA itanipa imani la sivyo ntarudi kijijini kwangu! Soka ni maisha yangu!”

No comments:

Powered By Blogger