Wednesday 21 October 2009

Fergie asusa Mkutano na Waandishi baada ya swali kuhusu Refa Wiley!!
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson aligoma kuendelea na mkutano wa Waandishi wa Habari uliokuwa ukifanyika Uwanjani Luzhniki huko Moscow, Urusi baada ya kuulizwa swali kuhusu kesi yake na FA iliyotokana na kauli yake kuwa Refa Alan Wiley hayuko fiti.
Ferguson amepewa na FA mpaka Novemba 3 kuwasilisha utetezi wake kuhusu mashitaka yanayohusiana na kesi hiyo.
Baada ya kuulizwa swali kuhusu Refa Alan Wiley, Ferguson aliinuka na kutoka chumba cha mahojiano baada ya kutamka: “Swali la kipumbavu na halipati jibu! Nipo kwenye mkutano huu kuhusu mechi na CSKA Moscow!”
Boro yamtimua Southgate!!!
Timu iliyoshushwa Daraja toka Ligi Kuu msimu uliopita, Middlesbrough, imemfukuza kazi Meneja wao Derek Southgate ambae walikuwa nae kwa miaka mitatu na nusu.
Klabu ya Middlesbrough pia imetamka msaidizi wake Alan Smith nae ameondolewa na Makocha Colin Cooper na Steve Agnew watakaimu nafasi ya Umeneja kwa muda.
Klabu hiyo ipo Ligi ya Coca Cola Championship iliyo chini tu ya Ligi Kuu England.
Derek Southgate alichukua wadhifa wa Umeneja baada ya Meneja aliekuwepo Steve McClaren kuteuliwa kuwa Meneja wa England.
Kabla ya uteuzi huo wa kuwa Meneja wa Boro, Southgate alikuwa ni Mchezaji wa klabu hiyo akicheza kama Sentahafu.

No comments:

Powered By Blogger