Sunday 11 October 2009

Wenger aambiwa muda wa kusubiri umekwisha, leta Kombe Emirates!!!
Arsene Wenger amejulishwa na Wamiliki wa Arsenal kuwa wamechoka kusubiri na msimu huu hamna subira na wanataka kuona Kombe linatua Uwanjani Emirates.
Tangu wachukue Kombe la FA mwaka 2005, Arsenal hawajanyakua tena Kombe lolote lile ingawa kosakosa ni nyingi na wana Kikosi cha Vijana wanaotandaza ‘Soka Tamu’ linalovutia Ulaya nzima.
Mkurugenzi Mtendaji wa Arsenal, Ivan Gazidis, amesema: “Ni lengo letu kuchukua Kikombe msimu huu! Kumaliza nafasi ya pili, tatu au nne si bora kwetu! Tuna imani tuna Kikosi kizuri!”
Gazidis, mwenye asili ya Afrika Kusini, aliingizwa kwenye Bodi ya Wakurugenzi ya Arsenal Novemba 2008, amesisitiza kuwa ingawa Soka ni biashara kubwa haiwezi kusahaulika kuwa Arsenal wapo hapo kwa ajili ya Mashabiki wao ambao hawajali Mahesabu mazuri ya Fedha bali hutaka ushindi uwanjani.
NANI KATINGA BONDENI 2010 JANA?
Ifuatayo ni taarifa nani ameingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwakani:
UNITED STATES (11 Oktoba, 2009)
USA walipata ushindi wa ugenini hapo jana walipowafunga Honduras 3-2 n kupata tiketi ya kwenda Afrika Kusini huku wakiwa na mechi moja mkononi.
MEXICO (11 Oktoba, 2009)
Mexico wamejihakikishia kucheza Fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya 14 huku wakiwa na mechi moja mkononi walipowafunga El Salvador 4-1 hapo jana.
CHILE (11 Oktoba, 2009)
Chile watatua Afrika Kusini baada ya kuifunga Colombia 4-2 na hii itakuwa ni mara yao ya kwanza tangu 1998.
ITALY (10 Oktoba, 2009)
Mabingwa Watetezi Italia walipata suluhu ya 2-2 ugenini huko Dublin, Ireland waliposawazisha bao dakika ya mwisho na kutinga Fainali za Kombe la Dunia kutetea taji lao.
SERBIA (10 Oktoba, 2009)
Serbia hapo jana waliwakung’uta Romania 5-0 mjini Belgrade na kuingia Fainali za 2010 huko bondeni.
DENMARK (10 Oktoba, 2009)
Baada ya kuwachomeka bao 1-0 Mahasimu wao wakubwa, Sweden, mjini Copenhagen, Denmark sasa wako Fainali huko Afrika Kusini.
GERMANY (10 Oktoba, 2009)
Tangu mwaka 1950, Germany hawajaikosa hata Fainali moja ya Kombe la Dunia na jana wakiwa ugenini huko Moscow, Urusi, waliwashinda Wenyeji wao Urusi bao 1-0 na kutinga Fainali kama desturi yao.
IVORY COAST (10 Oktoba, 2009)
Ivory Coast walitoka suluhu 1-1 na Malawi mjini Blantyre na hiyo ilikuwa tosha kuingia Fainali Afrika Kusini huku wakiwa na mechi moja mkononi.
LISTI KAMILI YA TIMU ZILIZOINGIA FAINALI YA 2010:
WENYEJI: South Africa
AFRICA: Ghana, Ivory Coast
ASIA: Australia, Japan, North Korea, South Korea
EUROPE: Denmark, England, Germany, Netherlands, Serbia, Spain, Italy
SOUTH AMERICA: Brazil, Paraguay, Chile
NORTH, CENTRAL AMERICA AND CARIBBEAN: United States, Mexico
MATOKEO MECHI ZA Oktoba 10:
Afrika:
Ivory Coast yaingia Fainali!
Zambia 0 v Egypt 1
Malawi 1 v Ivory Coast 1
Cameroun 3 v Togo 0
Gabon 3 v Morocco 1
Asia na Oceania:
Bahrain 0 New Zealand 0
[Marudio huko New Zealand]
MECHI ZA LEO Oktoba 11:
Benin v Ghana
Nigeria v Mozambique
Tunisia v Kenya
Guinea v Burkina Faso
Mali v Sudan
Algeria v Rwanda
Ulaya:
Oktoba 10:
Finland 2 v Wales 1
Luxemborg 0 v Switzerland 3
Belarus 4 v Kazakhstan 0
Russia 0 v Germany 1
Estonia 0 v Bosnia-Herzegovina 2
Montenegro 2 v Georgia 1
Ukraine 0 v England 1
Denmark 1 v Sweden 0
Liechtenstein 0 v Azerbaijan 2
Republic of Ireland 2 v Italy 2
Czech Republic 2 v Poland 0
Slovakia 0 v Slovenia 2
Austria 2 v Lithuania 1
Serbia 5 v Romania 0
Portugal 3 v Hungary 0
Belgium 2 v Turkey 0
Israel 3 v Moldova 1
Armenia 1 v Spain 2
France 5 v Faroe Islands 0
Greece 5 v Latvia 2
Marekani ya Kusini:
Oktoba 10:
Colombia 2 v Chile 4
Ecuador 1 v Uruguay 2
Venezuela 1 v Paraguay 2
Argentina 2 v Peru 1
Oktoba 11:
Bolivia v Brazil
FIFA U-20 WORLD CUP EGYPT 2009
Brazil na Costa Rica zatinga Nusu Fainali!!!
MATOKEO MECHI ZA Jumamosi, Oktoba 10:
Brazil 2 v Germany 1
UAE 1 v Costa Rica 2
NUSU FAINALI:
Oktoba 13:
Ghana v Hungary
Brazil v Costa Rica
FAINALI:
Oktoba 16

No comments:

Powered By Blogger