Thursday 15 October 2009

LIGI KUU ENGLAND KURUDI KILINGENI WIKIENDI!!!
Baada ya kuwa “mapumzikoni” kwa wiki mbili kupisha Mechi za Kimataifa za michuano ya Kombe la Dunia, wikiendi hii viwanja mbalimbali England vitawaka moto tena kwa mechi za Ligi Kuu England.
Mpaka sasa wakati karibu kila Timu imecheza mechi 8, Chelsea ndie alieshika uongozi akiwa na pointi 21 akifuatiwa na Mabingwa Watetezi Manchester United mwenye 19.
Nafasi ya 3 ipo kwa Tottenham mwenye pointi 16 sawa na Manchester City ingawa Man City wamecheza mechi moja pungufu.
Arsenal na Liverpool wamefungana kwa pointi 15 lakini Arsenal amecheza mechi 7 tu na Liverpool 8.
Mechi za Ligi Kuu zitafuatiwa na zile Mechi Kubwa za Ulaya za UEFA CHAMPIONS LEAGUE siku za Jumanne na Jumatano kwa Arsenal na Liverpool kucheza mechi zao Jumanne na Chelsea na Man U kucheza Jumatano.
RATIBA KAMILI:
LIGI KUU:
Jumamosi, Oktoba 17
Aston Villa v Chelsea [saa 8 na dak 45 mchana]
[saa 11 jioni]
Arsenal v Birmingham
Everton v Wolverhampton
Man United v Bolton
Portsmouth v Tottenham
Soke City v West Ham
Sunderland v Liverpool
Jumapili, Oktoba 18
[saa 9 mchana]
Blackburn v Burnley
Wigan v Man City
Jumatatu, Oktoba 19
[saa 4 usiku]
Fulham v Hull City
UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
[saa 3 dak 45 usiku]
Jumanne, 20 Oktoba 2009
AZ Alkmaar v Arsenal,
Barcelona v Rubin Kazan,
Debrecen v Fiorentina,
Inter Milan v Dynamo Kiev,
Liverpool v Lyon,
Olympiakos v Standard Liege,
Rangers v Unirea Urziceni,
VfB Stuttgart v Sevilla,
Jumatano, 21 Oktoba 2009
Bordeaux v Bayern Munich,
CSKA Moscow v Manchester United
Chelsea v Atletico Madrid,
FC Porto v Apoel Nicosia,
FC Zurich v Marseille,
Juventus v Maccabi Haifa,
Real Madrid v AC Milan,
Wolfsburg v Besiktas,

No comments:

Powered By Blogger