Hata hivyo, Fellaini aliondoka Kambini na kwenda kutibiwa jino lake.
Kitendo hicho cha Fellaini kimewaudhi KBVB na kimewatumia faksi Everton kuwajulisha watatumia sheria ya FIFA inayowapa uwezo kumpiga marufuku Mchezaji huyo kuchezea Klabu yake kwa siku 5 baada ya mechi inayohusu Nchi yake ambayo amejitoa Kikosini.
Endapo KBVB itamfungia Fellaini kwa siku hizo 5 basi hataweza kuichezea Everton kwenye mechi ya Ligi Kuu Jumamosi dhidi ya Wolverhampton Wanderers.
Everton imelalamika kuhusu hatua hiyo ya KBVB na kusema wao kama Klabu hawahusiki kwenye mzozo wa Mchezaji huyo binafsi na Nchi yake.
Megson amtetea Fergie!!
Kocha wa Bolton Wanderers, Gary Megson, ambayo Timu yake itapambana na Manchester United kwenye mechi ya Ligi Kuu hapo Jumamosi, amemtetea Sir Alex Ferguson wa Man U katika mzozo unaoihusu kauli ya Ferguson kusema Refa Alan Wiley aliechezesha mechi ya Man U na Sunderland ‘hayuko fiti’ na kusababisha Chama cha Marefa kumjia juu na pia FA kumtaka Ferguson ajieleze.
Megson amesema: “Wanamwandama kwa vile ni mtu mwenye jina kwenye Soka! Ameomba radhi lakini kila mtu analaumu hata huko kuomba radhi kwake! Asingeomba radhi wangemsema, kaomba radhi wanamsema! Sasa afanyeje? Ameomba radhi huo ungekuwa mwisho wa mzozo!”
Mpaka sasa Sir Alex Ferguson binafsi hajazungumza lolote sakata hilo kwa vile yuko safarini huko New York, Marekani.
No comments:
Post a Comment