Saturday 10 October 2009

Capello: ‘Tunataka ushindi leo!’
Ingawa England imeshafaulu kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwakani baada ya kushinda mechi zao zote 8 katika Kundi lao na bado wakiwa na mechi 2 mkononi mojawapo ikichezwa ugenini leo na Ukraine, Kocha wa England, Fabio Capello ametaka Timu yake isibweteke na icheze kwa moyo wa ushindi.
Capello alisema: “Timu lazima icheze kwa moyo uleule! Ntachagua Kikosi bora! Mechi hii ni muhimu kuijenga Timu iwe bora!”
Timu ya Capello itatokana na :
MAKIPA: Paul Robinson (Blackburn), Robert Green (West Ham), David James (Portsmouth)
WALINZI: Ashley Cole (Chelsea), John Terry (Chelsea), Glen Johnson (Liverpool), Wayne Bridge (Manchester City), Joleon Lescott (Manchester City), Wes Brown (Manchester United), Rio Ferdinand (Manchester United), Matthew Upson (West Ham).
VIUNGO: James Milner (Aston Villa), Frank Lampard (Chelsea), David Beckham (Los Angeles Galaxy), Steven Gerrard (Liverpool), Gareth Barry (Manchester City), Shaun Wright-Phillips (Manchester City), Michael Carrick (Manchester United), Aaron Lennon (Tottenham)
WASHAMBULIAJI: Gabriel Agbonlahor (Aston Villa), Emile Heskey (Aston Villa), Peter Crouch (Tottenham), Carlton Cole (West Ham), Wayne Rooney (Manchester United)
Uruguay waibiwa huko Ecuador!!!
Timu ya Taifa ya Uruguay imelalamika kuwa imeibiwa Mipira, Viatu na Jezi hotelini mwao Nchini Ecuador ambako leo wanapambana na Ecuador kwenye mechi muhimu ya Kombe la Dunia huku Timu zote zikiwania kunyakua nafasi mbili zilizosalia kati ya 4 za Nchi za Marekani ya Kusini kuingia Fainali.
Wakati tayari Brazil na Paraguay zipo Fainali huku nafasi 2 zikibaki pambano lao la leo ni muhimu sana kwani Uruguay wapo nafasi ya 6 wakiwa na pointi 21 na Ecuador wako nafasi ya 4 wakiwa na pointi 23.
Timu hizi zilitoka 0-0 mechi ya kwanza Nchini Uruguay. Eduardo Di Maggio, Mkuu wa Vifaa vya Uruguay, aliwajulisha Polisi wa Mji wa Guayaqil, Ecuador walipofikia Uruguay, kuhusu tukio hilo la wizi.
Urguay walifikia Guayaqil mapema ili kujizoeza hali ya hewa kabla ya kusafiri kwenda Quito Mji ulio Futi zaidi ya Elfu 7 toka usawa wa bahari hali inayofanya kupumua kuwe ni kwa shida kwa ajili ya hewa kuwa nyepesi na upungufu wa Oksejeni.
FIFA U-20 WORLD CUP EGYPT 2009
Wawikilishi pekee wa Ghana kwenye Kombe la Dunia kwa Vijana Chini ya Miaka 20 jana waliifunga South Korea mabao 3-2 na kuingia Nusu Fainali.
Nusu Fainali Ghana watakutana na Hungary walioitoa Italy 3-2 baada ya dakika 120 kufuatia mechi kuwa 1-1 kwenye dakika 90 za kawaida.
ROBO FAINALI:
09/10/09: South Korea 2 v Ghana 3
09/10/09: Italy 2 v Hungary 3
MECHI ZA LEO Jumamosi, Oktoba 10:
10/10/09: Brazil v Germany
10/10/09: UAE v Costa Rica
NUSU FAINALI:
Oktoba 13:
Ghana v Hungary
Brazil/Germany v UAE/Costa Rica
FAINALI:
Oktoba 16:

No comments:

Powered By Blogger