Sunday 4 October 2009

Mechi ya Wababe wa Scotland: Rangers 2 Celtic 1
Leo, Rangers imeibwaga Celtic 2-1 katika "dabi" iliyochezwa Uwanjani kwa Rangers Ibrox Stadium mjini Glasgow katika mechi ya Ligi Kuu ya Scotland.
Ni Mshambuliaji Kenny Miller wa Rangers ndie aliekuwa shujaa baada ya kupachika bao 2 katika dakika ya 8 na 16.
Bao la Celtic lilifungwa kwa penalti dakika ya 25 na McGeady.
Celtic bado anaongoza Ligi hiyo kwa kuwa na pointi 16 huku Rangers wana 15 kwa mechi 7 kwa kila Timu.

No comments:

Powered By Blogger