Friday 19 March 2010

EUROPA LIGI: Fulham v Wolfsburg na Liverpool v Benfica
Timu za England, Fulham na Liverpool, zimetenganishwa na zitakuta tu kwenye Fainali endapo zitafuzu kuvuka vikwazo vya Robo Fainali kwenye Mashindano ya EUROPA LIGI.
Kwenye Robo Fainali, Fulham watacheza na Wolfsburg ya Ujerumani. Mshindi wa mechi hii atacheza na Mshindi wa mechi kati ya Hamburg v Standard Liege kwenye Nusu Fainali.
Nao Liverpool wataivaa Benfica ya Ureno kwenye Robo Fainali na Mshindi wa mechi hii atacheza na Mshindi wa Valencia v Atletico Madrid kwenye Nusu Fainali.
Robo Fainali zitachezwa Aprili 1 na marudio Aprili 8.

No comments:

Powered By Blogger