Monday 15 March 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Jumanne na Jumatano kimbembe cha kuingia Robo Fainali!!
RATIBA [Mechi za marudiano]
Jumanne, 16 Machi 2010
Chelsea v Inter Milan
Sevilla v CSKA Moscow
Jumatano, 17 Machi 2010
Barcelona v VfB Stuttgart
Bordeaux v Olympiakos
MATOKEO MECHI ZA KWANZA:
Olympiakos 0 v Bordeaux 1
VfB Stuttgart 1 v Barcelona 1
CSKA Moscow 1 v Sevilla 1
Inter Milan 2 v Chelsea 1
Timu tayari ziko Robo Fainali:
-Arsenal
-Bayern Munich
-Manchester United
-Lyon
TATHMINI:
Siku ya Jumanne Machi 16, Chelsea inahitaji kumfunga Inter Milan japo bao 1-0 ili itinge Robo Fainali kwa vile Chelsea alipigwa 2-1 na Inter Milan katika mechi ya kwanza.
Katika mechi nyingine ya siku ya Jumanne ni marudiano ya Sevilla na CSKA Moscow na suluhu ya 0-0 ni tosha kwa Sevilla kufuzu Robo Fainali.
Lakini, kwa vile vile Timu hizo zilitoka 1-1 kwenye mechi ya kwanza, sare ya zaidi ya mabao 1-1 ni nzuri kwa CSKA kwani watapita kwa wingi wa mabao ya ugenini.
Jumatano ni marudio kati ya Barcelona v VfB Stuttgart na Bordeaux v Olympiakos.
Katika mechi ya Barcelona v VfB Stuttgart, hali ni kama ya mechi ya Sevilla na CSKA Moscow kwani Barcelona anahitaji sare ya 0-0 apite lakini sare ya magoli zaidi ya 1-1 ni nzuri kwa VfB Stuttgart.
Bordeaux wao wanahitaji sare ya aina yoyote ili waibwage Olympiakos kwa vile walishinda 1-0 ugenini.
Ili Olympiakos apite ni lazima aifunge Bordeaux bao 2 au apate ushindi wowote wa bao zaidi ya 2.

No comments:

Powered By Blogger